Page 74 - Historiayatznamaadili
P. 74

Sayansi na teknolojia ya ufumaji ilifanywa kwa kufuma na kusuka
              makuti, matete au majani ya mianzi ili kupata umbo fulani.
              Kielelezo namba 22, kinaonesha makuti yaliyosukwa.


          FOR ONLINE READING ONLY






















                               Kielelezo namba 22: Makuti yaliyosukwa

                                Kazi ya kufanya namba 11


                           Jadili namna ya kuendeleza sayansi na teknolojia
                           ya ususi katika jamii zetu kwa maendeleo ya sasa.




              Sayansi na teknolojia asilia ya uchongaji

              Sayansi na teknolojia ya asili ya uchongaji ilihusisha uchongaji
              wa vifaa kama vile vinu, michi, bakuli, vijiko, sahani, miko, upawa,
              meza, vigoda, chanuo, mipini, vitanda, viti na marimba za muziki.
              Pia, ulihusisha uchongaji wa vyombo vya usafiri kwenye maji

              mfano, majahazi, mitumbwi, ngalawa na makasia. Mfano wa
              jamii zilizofanya shughuli za uchongaji wa vitu mbalimbali ni
              Wamakonde, Wagogo, Wakimbu, Wanyamwezi, Wayao na
              Waha. Jamii za Wayao na Wamakonde zilijihusisha zaidi na

              uchongaji wa vitu vilivyotumika kwa mapambo.

              Sayansi na teknolojia ya uchongaji ilitumia maarifa na ujuzi




                                                   67




                                                                                          06/11/2024   11:30:03
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   67
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   67                                     06/11/2024   11:30:03
   69   70   71   72   73   74   75   76   77   78   79