Page 79 - Historiayatznamaadili
P. 79

Sayansi na teknolojia ya tiba za asili
              Sayansi na teknolojia ya tiba ya asili zilitofautiana kutoka jamii
              moja na nyingine. Sayansi na teknolojia ya tiba za asili zilitumia
              mimea na wanyama ili kutayarisha dawa.  Sehemu ya mimea
          FOR ONLINE READING ONLY
              iliyotumika ni mizizi, mbegu, majani, magome ya miti na maua.
              Kielelezo namba 26, kinaonesha baadhi ya sehemu za mimea
              na wanyama zilizotumika kutengeneza dawa za asili.



















              Kielelezo namba 26: Sehemu za mimea na wanyama zilizotumika
                                        kutengenezea dawa za asili

              Sehemu kubwa ya mimea hii ilipatikana katika mazingira ya jamii
              husika. Sayansi na teknolojia ya utayarishaji dawa ilifanyika
              kwa kuchukua mmea husika, kisha kuuchemsha, kuukausha,
              kuuponda, kuutwanga, kuusaga, kuuchoma, au kuukwangua ili

              kupata dawa. Pia, mmea ulichanganywa na maji, uji au supu na
              kuchemshwa ili kupata dawa. Sayansi na teknolojia ya asili ya
              utengenezaji dawa ilitumika ili kuifanya mitishamba hiyo iweze
              kutibu kwa njia mbalimbali.

              Dawa zilizotengenezwa kutokana na wanyama zilipatikana

              kwa kuchemsha na kuchuja mafuta kutoka katika nyama
              yenye mafuta, na mafuta hayo kutumika kama tiba. Pia, nyama
              ilichemshwa ili kupata supu, ambayo ilitumika kama dawa.

              Matumizi ya dawa yalitegemea aina ya dawa na ugonjwa husika.

              Zipo dawa zilizotumika kama vimiminika baada ya kuchemshwa
              na nyingine zilitumika katika hali ya unga. Dawa zilizochomwa
              zilitumika katika hali ya majivu au mkaa.


                                                   72




                                                                                          06/11/2024   11:30:08
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   72
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   72                                     06/11/2024   11:30:08
   74   75   76   77   78   79   80   81   82   83   84