Page 80 - Historiayatznamaadili
P. 80

Maadili katika sayansi na teknolojia asilia za tiba za asili
              Sayansi na teknolojia ya utayarishaji wa dawa za asili ulifanywa
              kwa kuzingatia maadili ambayo msingi wake ulikuwa ni wa siri
              sana. Usiri ulifanyika ili kuficha utaalamu kwa baadhi ya watu
          FOR ONLINE READING ONLY
              ambao walijulikana kama waganga. Si kila mtu katika jamii alijua
              namna ya kutengeneza dawa za asili. Uwezo wa kutengeneza
              dawa ulikuwa kwa baadhi ya watu kwenye jamii. Wataalamu
              wa tiba asili walirithisha ujuzi wao kwa watu waliowachagua.
              Pia, utunzaji wa siri ulilenga kujali na kulinda utu wa wagonjwa.

              Uadilifu, upendo na huruma vilikuwa miongoni mwa maadili

              yaliyozingatiwa katika tiba asili. Sifa hizi zilikuwa za msingi kwa
              kuwa tiba za asili zilihitaji wataalamu walio waadilifu. Tiba za asili
              hazikuwa kwa ajili ya biashara katika jamii za kale, bali zilitolewa
              kama huduma kwa wahitaji. Wagonjwa walitoa chochote kama
              shukurani na haikuwa lazima. Pia, usafi ulizingatiwa katika
              kutayarisha dawa hizi. Palikuwapo na kanuni maalumu za
              utayarishaji wa kila dawa na matumizi yake.  Mfano, palikuwepo

              na dawa zilizotumika kwa kunywa, kuoga, kupaka, kunusa,
              kujifukiza na za kuchanjiwa. Kimsingi, matumizi ya tiba za asili
              yaliwezesha jamii kutibu magonjwa tofauti.

                      Zoezi namba 5


                1.  Taja faida za matumizi ya tiba za asili katika jamii.

                2.  Ainisha sayansi na teknolojia za tiba zilizotumika
                      kutengeneza dawa za asili.

                3.  Eleza maadili yaliyozingatiwa katika sayansi ya tiba za
                      asili katika jamii za kale.



                                Kazi ya kufanya namba 14

                           Fanya uchunguzi kuhusu mwendelezo wa sayansi
                           na teknolojia ya tiba za asili katika jamii yako kwa

                           sasa.



                                                   73




                                                                                          06/11/2024   11:30:08
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   73
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   73                                     06/11/2024   11:30:08
   75   76   77   78   79   80   81   82   83   84   85