Page 81 - Historiayatznamaadili
P. 81
Sayansi na teknolojia asilia ya kutengeneza nguo
Jamii za kale zilikuwa na nguo za asili zilizotengenezwa kwa
kutumia ngozi za wanyama na magome ya miti. Magome ya miti
yalibanduliwa kutoka katika miti maalumu iliyotumika kutengeneza
FOR ONLINE READING ONLY
nguo. Sayansi na teknolojia ya kutengeneza nguo ilifanywa kwa
kupondaponda magome ya miti
kwa kutumia jiwe, vipande vya
miti au kitu kigumu ili kuyalainisha
na kupata nguo. Nguo hizi
zilijulikana kama “mbungu” katika
jamii za Wahaya. Pia, nguo za
magome ya miti zilikuwapo katika
jamii za Wamanyema, Waha, na
Wahangaza. Kielelezo namba 27,
kinaonesha magome ya miti
yaliyotumika kutengenezea nguo. Kielelezo namba 27: Magome
ya miti ya kutengenezea nguo
Vilevile, ngozi za wanyama zilichunwa na kuanikwa, kisha
kuzilainisha kwa kupondaponda na kupaka mafuta ili kupata
nguo. Kielelezo namba 28, kinaonesha nguo za magome ya
miti na ngozi za wanyama.
Nguo za magome ya miti Nguo za ngozi ya wanyama
Kielelezo namba 28: Nguo za magome ya miti na ngozi za wanyama
74
06/11/2024 11:30:10
Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd 74
Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd 74 06/11/2024 11:30:10