Page 84 - Historiayatznamaadili
P. 84

kufuma nyavu na kusuka mitego ya samaki ambayo
                    iliendeleza uvuvi. Zana za chuma ziliwaibua mafundi wa
                    kuchonga ambao walichonga vyombo vya nyumbani kama
                    vile sahani, bakuli, vinu, miko na pawa. Pia, walichonga
                    vyombo vya uvuvi na usafiri kama mitumbwi na ngalawa;
          FOR ONLINE READING ONLY
              (c)  Kuongezeka kwa uzalishaji wa ziada wa bidhaa
                    mbalimbali ndani na nje ya jamii.  Ongezeko la bidhaa
                    lilisababisha watu kuanza kubadilishana bidhaa. Huu ukawa
                    ndio mwanzo wa watu kufanya biashara. Jamii za wakulima
                    zilibadilishana mifugo kwa nafaka kutoka kwa jamii za
                    wafugaji. Pia, wafugaji na wakulima walibadilisha bidhaa
                    zao ili kupata zana kutoka kwa mafundi sanifu; na

              (d)  Kuimarika kwa afya ya jamii. Wataalamu wa tiba asilia
                    waliwatibu wagonjwa waliokuwepo kwenye jamii. Udhibiti
                    wa magonjwa ulisababisha jamii kuwa na afya na kuweza
                    kushiriki katika shughuli mbalimbali za uchumi. Uwepo wa
                    tiba asilia na wataalamu wake kama wakunga, kuliwezesha
                    akina mama kujifungua salama. Uzazi salama ulisababisha
                    ongezeko la watu ambao ndiyo nguvu kazi katika jamii.
                    Hivyo, kuendeleza uchumi wa jamii.

              Sayansi na teknolojia za asili zilichangia maendeleo endelevu ya
              uchumi nchini kabla ya kuja kwa wakoloni. Sayansi na teknolojia
              zilisimamia utunzaji wa mazingira na kuhimiza maadili ya jamii.

              Hii ilisaidia kutunza mazingira kwa vizazi vijavyo, kukinga jamii
              na magonjwa, kuongeza nguvu kazi na kuhifadhi utaalamu katika
              jamii. Matumizi ya sayansi na teknolojia asilia yalisaidia kuleta
              maendeleo ya uchumi  na jamii ya muda mrefu.

                                Kazi ya kufanya namba 15


                           Jadili wajibu wa jamii katika kuendeleza sayansi na
                           teknolojia  za asili kwa sasa.











                                                   77




                                                                                          06/11/2024   11:30:10
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   77                                     06/11/2024   11:30:10
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   77
   79   80   81   82   83   84   85   86   87   88   89