Page 87 - Historiayatznamaadili
P. 87

Sura ya              Shughuli za uchumi


                      Nne                   kabla ya ukoloni


          FOR ONLINE READING ONLY

                  Utangulizi


                Jamii za Kitanzania zilikuwa na shughuli mbalimbali za uchumi kabla ya kuja
                kwa wakoloni. Katika sura hii, utajifunza kuhusu shughuli za uchumi kama

                vile kilimo, uhunzi, ususi, ufinyanzi, uvuvi na maadili yake. Pia, utajifunza
                mchango wa shughuli hizo za uchumi katika maendeleo ya jamii nchini
                kabla ya ukoloni. Vilevile, utajifunza wajibu wa jamii katika kuendeleza
                shughuli za uchumi. Umahiri utakaoupata utakusaidia kutambua shughuli
                za uchumi na michango yake katika maendeleo ya jamii nchini, hivyo,

                kuweza kuzithamini na kuziendeleza katika jamii zetu kwa sasa.



                            Fikiri

                            Shughuli za uchumi nchini na maadili yake kabla

                            ya ukoloni.


              Dhana ya shughuli za uchumi

                                Kazi ya kufanya namba 1

                           Fanya uchunguzi kwa kuuliza au kutembelea maeneo

                           yenye shughuli za uchumi zilizofanyika katika jamii
                           inayokuzunguka kabla ya ukoloni.


              Jamii zilijishughulisha na shughuli mbalimbali za uchumi kabla
              ya ukoloni. Shughuli hizo ni kilimo, uvuvi, biashara, viwanda

              na kadhalika.  Shughuli hizo zilitofautiana kati ya jamii moja na
              nyingine. Hii ilitokana na utofauti wa mazingira ya kijiografia
              ambapo jamii iliishi, hali ya hewa, uwapo wa rasilimali asilia na
              maarifa na ujuzi wa asili katika jamii husika.



                                                   80




                                                                                          06/11/2024   11:30:10
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   80
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   80                                     06/11/2024   11:30:10
   82   83   84   85   86   87   88   89   90   91   92