Page 92 - Historiayatznamaadili
P. 92

samaki kutoka kwa jamii za wasusi. Vilevile, walibadilishana
              samaki na jamii za wachongaji ili kupata mitumbwi na ngalawa
              iliyotumika katika uvuvi. Hali kadhalika walibadilishana samaki
              ili kupata chumvi kutoka kwa jamii zilizotengeneza chumvi. Hii
          FOR ONLINE READING ONLY
              ilisaidia kukua kwa shughuli za uchumi na biashara kabla ya
              ukoloni. Kimsingi, palikuwa na maendeleo makubwa katika
              shughuli za uvuvi kabla ya kuja kwa wakoloni.


                                Kazi ya kufanya namba 4


                           Jadili na kuandika mambo yaliyochangia kukua kwa
                           shughuli za uvuvi kabla ya ukoloni.





              Wavuvi hoyee! Watu wote kwenye hadhara waliitikia hoyee!
              Kisha kupiga makofi na vigelegele. Wageni walifurahi sana
              kusikia kuhusu maendeleo hayo ya uvuvi.


                      Zoezi namba 2

                1.  Je, ni maendeleo yapi yaliyokuwapo katika shughuli za
                      uvuvi kabla ya ukoloni?

                2.  Eleza namna ya kuendeleza matumizi ya zana za uvuvi
                      na mbinu za uvuvi na uhifadhi wa samaki kwa sasa.



              Shughuli za uchumi katika viwanda
              Wageni kutoka jamii zilizojishughulisha na viwanda walieleza
              kuhusu maendeleo ya shughuli zao kabla ya ukoloni. Shughuli
              za uchumi katika viwanda zilihusu uhunzi, ufinyanzi, uchongaji,
              ususi na utengenezaji chumvi.


              Shughuli za uchumi katika uhunzi

              Mzee Paukwa alielezea zaidi maendeleo ya shughuli za viwanda
              zilizotokana na uhunzi. Mzee Paukwa alianza kwa kuelezea
              kwamba:




                                                   85




                                                                                          06/11/2024   11:30:12
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   85
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   85                                     06/11/2024   11:30:12
   87   88   89   90   91   92   93   94   95   96   97