Page 95 - Historiayatznamaadili
P. 95

Kazi ya kufanya namba 6

                           Jadili namna ya kuendeleza shughuli za ufinyanzi

                           nchini kwa sasa ili kukuza uchumi wa viwanda.
          FOR ONLINE READING ONLY


              Wafinyanzi hoyee! Alisema bibi Mkisi na kuhitimisha simulizi yake.
              Hoyee! Wageni waliitikia huku wakipiga vigelegele na makofi.


              Alifuata Mzee Pakawa wa kabila la Wandali ambaye alieleza
              kuhusu shughuli za viwanda vya ususi.


              Shughuli za uchumi za ususi
              Mzee Pakawa alianza simulizi kwa kuelezea kuwa:

              Jamii nyingi zilikuwa na maendeleo katika shughuli za viwanda
              vya ususi. Viwanda vya ususi vilitengeneza vitanda vya kamba,
              nyungo, nyavu za kuvulia samaki, vikapu, mikeka na kadhalika.
              Vitu hivi vilitengenezwa kwa ajili ya shughuli  za uchumi na
              matumizi ya nyumbani. Mzee Pakawa alionesha mfano wa
              vikapu  vilivyotengenezwa katika  viwanda  vya ususi  kama

              vinavyoonekana katika Kielelezo namba 4.

















                                      Kielelezo namba 4:  Vikapu
              Shughuli za ususi zilifanyika kwa kutumia ukindu, miwaa, makuti
              na mianzi. Pia, viwanda vya ususi vilitengeneza nyavu ambazo
              zilitumika kama mitego ya kutegea wanyama na ya kuvulia
              samaki. Mitego ilitengenezwa kwa kutumia nyuzi laini.  Usukaji
              wa bidhaa hizi ulitumia matete, miwaa, mianzi na makuti. Jamii



                                                   88




                                                                                          06/11/2024   11:30:13
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   88                                     06/11/2024   11:30:13
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   88
   90   91   92   93   94   95   96   97   98   99   100