Page 90 - Historiayatznamaadili
P. 90

Shughuli za kilimo ziliambatana na uwepo wa maarifa na stadi za
              kukuza na kuimarisha kilimo. Mfano, wakulima walifanya kilimo
              cha matuta na ngoro ili kuzuia mmomonyoko wa udongo. Pia,
              maeneo ya Engaruka, palikuwapo na kilimo cha umwagiliaji.
          FOR ONLINE READING ONLY
              Kilimo cha umwagiliaji kilifanyika kwa kuvuna maji ya mvua na
              kuyatumia wakati wa ukame. Jamii za Wachaga pia zilifanya
              kilimo cha umwagiliaji kwa kuweka mitaro ambayo ilitiririsha maji
              kutoka maeneo yenye maji hadi kwenye mashamba kwa ajili ya

              kilimo cha umwagiliaji. Kimsingi, jamii zilikuwa na maendeleo
              makubwa katika shughuli za kilimo. Jamii zililima mazao kwa ajili
              ya chakula na ziada. Ziada ilitumika kwa ajili ya kubadilishana
              na jamii nyingine ili kupata bidhaa zingine. Jamii za wakulima

              zilipata vitu kama vyungu, chumvi, zana za chuma na kadhalika.


              Wakulima hoyee! Watu wote kwenye hadhara waliitikia hoyee!
              Kisha kupiga makofi na vigelegele. Wageni walifurahi sana
              kusikia kuhusu maendeleo katika kilimo.


                                Kazi ya kufanya namba 2

                           Jadili na kuandika mambo uliyojifunza kuhusu

                           shughuli za kilimo kabla ya ukoloni.





                      Zoezi namba 1


                1.  Eleza maendeleo yaliyokuwapo katika kilimo kabla ya
                      ukoloni.

                2.  Ainisha mambo ya kuendeleza katika shughuli za kilimo
                      kwa sasa.



              Shughuli za uchumi katika uvuvi

              Mgeni aliyefuata alikuwa mzee Kwere ambaye alizungumzia
              shughuli za uchumi katika uvuvi. Mzee Kwere alieleza kuwa:


                                                   83




                                                                                          06/11/2024   11:30:12
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   83                                     06/11/2024   11:30:12
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   83
   85   86   87   88   89   90   91   92   93   94   95