Page 89 - Historiayatznamaadili
P. 89

uwepo wa sayansi na teknolojia katika matumizi ya zana za
              kilimo.  Mwanzoni, kilimo kilifanyika kwa kiwango kidogo. Hali
              hii ilitokana na uwepo wa zana duni za mawe na miti. Aidha,
              kadiri zana za kilimo zilivyoboreshwa, ndivyo, shughuli za kilimo
          FOR ONLINE READING ONLY
              zilivyoboreshwa.  Kielelezo namba 2, kinaonesha majembe ya
              miti yaliyotumika awali kwa shughuli za kilimo.






















                                 Kielelezo namba 2: Majembe ya miti

              Shughuli za kilimo zilishika kasi wakati wa ugunduzi wa chuma.
              Ugunduzi wa chuma ulisababisha utengenezaji wa zana za
              chuma kama vile majembe, mundu, mashoka na mapanga. Jamii
              zililima eneo kubwa zaidi kwa kutumia zana hizi.  Mfano, katika
              maeneo ya Kagera kulikuwa na wakulima walioimarika kutokana
              na matumizi ya zana za chuma katika kilimo. Wakulima hawa
              walimiliki ardhi kubwa na kuikodisha kwa watu wengine kwa ajili
              ya kilimo. Hali hii ilisababisha kukua kwa mfumo wa ukabaila

              uliojulikana kama “Nyarubanja”. Wakulima wakubwa waliomiliki
              ardhi walijulikana kama “Batwazi”. Pia palikuwapo na “Batwana”,
              ambao hawakumiliki ardhi. Batwana waliishi kwa kulima maeneo
              ya ardhi za Batwazi, kisha kuwapa Batwazi sehemu ya mazao
              waliyovuna kama ushuru. Pia, jamii za Wachaga, Wapare,
              Wasukuma na Wanyakyusa zilikuwa zimepiga hatua kubwa
              katika shughuli za kilimo kabla ya kuja kwa wakoloni. Jamii

              zililima mazao kama vile maharagwe, mtama, uwele, ulezi,
              magimbi na ndizi.



                                                   82




                                                                                          06/11/2024   11:30:11
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   82
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   82                                     06/11/2024   11:30:11
   84   85   86   87   88   89   90   91   92   93   94