Page 88 - Historiayatznamaadili
P. 88

Shughuli za uchumi za jamii kabla ya ukoloni
              Siku moja kiongozi wa jamii ya wakundi alifanya sherehe kubwa
              ambayo alialika watu kutoka jamii zilizojishughulisha na shughuli

              mbalimbali za uchumi. Hafla hii ilikuwa kwa ajili ya kuzitambua
          FOR ONLINE READING ONLY
              shughuli za kiuchumi zilizofanyika katika jamii zao na maadili
              yake. Wageni waalikwa walikaa karibu na moto mkubwa

              wakichoma nyama huku wakizungumzia kuhusu shughuli za
              uchumi katika jamii zao kabla ya kuja kwa wakoloni. Kielelezo
              namba 1, kinaonesha wageni toka jamii mbalimbali na bidhaa
              zitokanazo na shughuli zao za uchumi.
































                         Kielelezo namba 1:  Wageni kutoka jamii mbalimbali
              Shughuli za uchumi katika kilimo

              Mgeni wa kwanza kuzungumza alikuwa mzee Mwaka ambaye
              alizungumzia kuhusu shughuli za kilimo. Mzee Mwaka alianza

              kwa kuelezea kwamba:

              Shughuli ya uchumi katika jamii yetu ilikuwa kilimo. Shughuli
              za uchumi za kilimo zilitofautiana katika jamii za  wakulima

              kulingana na mazingira, maarifa na ujuzi wa stadi za kilimo na



                                                   81




                                                                                          06/11/2024   11:30:11
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   81                                     06/11/2024   11:30:11
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   81
   83   84   85   86   87   88   89   90   91   92   93