Page 83 - Historiayatznamaadili
P. 83

salama, na ile ambayo haina harufu mbaya, ladha chungu
                    au yenye sumu. Wavuvi, hali kadhalika, walitumia nyenzo
                    salama kama nyavu, madema na ndoano ili kutunza mazao
                    ya samaki. Uhunzi ulifanyika mbali na makazi ya watu ili
                    kuzuia watu wasivute hewa chafu iliyotokana na moshi wa
          FOR ONLINE READING ONLY
                    uyeyushaji chuma. Wanawake wajawazito hawakuruhusiwa
                    kuwa maeneo yenye tanuri la kuyeyushia chuma. Mwiko
                    huu uliwekwa ili kulinda afya ya wanawake kwa sababu
                    matanuru yalikuwa na joto kali ambalo ni hatari kwa afya
                    ya mama na mtoto awapo tumboni; na
              (g)  Matumizi ya sayansi na teknolojia yenye faida kwa jamii.
                    Hili lilizingatiwa kwa sababu teknolojia ilitokana na maarifa,
                    ujuzi na rasilimali asilia. Hivyo, jamii inayohusika ilikuwa
                    na haki ya kufaidika na teknolojia husika. Kwa mfano,
                    wataalamu wa tiba asilia hawakujitengenezea faida kwa
                    huduma walizotoa. Watu waliopatiwa tiba walitoa mifugo,
                    mazao au zana kama sehemu ya shukurani. Ubadilishanaji
                    wa mazao ya sayansi na teknolojia ulizingatia haki, usawa
                    na makubaliano.

              Mchango wa sayansi na teknolojia asili katika uchumi

              Sayansi na teknolojia za asili zilikuwa na mchango mkubwa kwa
              maendeleo ya uchumi katika jamii za kale. Sayansi na teknolojia
              za asili ziliendeleza uchumi kwa njia zifuatazo:
              (a)  Kuongeza ufanisi katika uzalishaji mali. Mfano, uvumbuzi
                    wa sayansi na teknolojia ya chuma, uliongeza ubora wa zana
                    katika kilimo, uwindaji na uvuvi. Wakulima walianza kulima
                    mazao katika eneo kubwa zaidi. Hii ilisaidia kupata mazao
                    mengi kwa ajili ya chakula na ziada ambazo zilitumika katika
                    biashara. Biashara ilizisaidia jamii kupata bidhaa ambazo
                    hawakuwanazo. Pia, kilimo kilisababisha ongezeko la idadi
                    ya watu kutokana na kuwapo kwa chakula cha kutosha na
                    lishe bora. Hii ilisababisha kuongezeka kwa nguvukazi.
                    Pia, zana hizo ziliongeza mazao katika uvuvi na uwindaji;
              (b)  Kuibua mafundi katika nyanja mbalimbali. Mafundi
                    hawa walikuwa tegemeo la wazalishaji mali wengine kwa
                    kuwatengenezea zana za kazi. Kwa mfano, wasusi waliweza



                                                   76




                                                                                          06/11/2024   11:30:10
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   76                                     06/11/2024   11:30:10
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   76
   78   79   80   81   82   83   84   85   86   87   88