Page 82 - Historiayatznamaadili
P. 82

Maadili katika sayansi na teknolojia asilia kabla ya ukoloni
              Jamii za kale zilizingatia maadili katika sayansi na teknolojia
              za asili. Miiko, kanuni na taratibu ziliwekwa na jamii katika

              utayarishaji, matumizi na mwendelezo wa sayansi na teknolojia
          FOR ONLINE READING ONLY
              asilia ndani ya jamii. Maadili haya yaliheshimu mifumo ya maarifa
              na ujuzi asilia, ibada na utamaduni wa jamii. Maadili yalizingatia:

              (a)  Kurithishwa maarifa na stadi kwa vizazi na vizazi. Hii
                    ilisaidia mwendelezo wa sayansi na teknolojia ya asili kwa
                    vizazi vijavyo;

              (b)  Mgawanyo wa maarifa na ujuzi katika jamii. Hii ilizingatia
                    zaidi mazingira na uwepo wa rasilimali maalumu katika
                    jamii. Mfano, wapo waliojifunza uhunzi, uvuvi, uchongaji,
                    ususi, tiba asilia  na kadhalika;
              (c)  Heshima. Jamii ziliheshimu maarifa na stadi katika sayansi
                    na teknolojia za asili. Jamii zilitambua uwapo wa wataalamu
                    na mafundi katika nyanja mbalimbali za sayansi na teknolojia
                    asilia;

              (d)  Ushirikiano na uhusiano katika utendaji wa kazi.
                    Ushirikiano na uhusiano ulifanyika ili jamii kunufaika na
                    sayansi na teknolojia toka jamii zingine;

              (e)  Utunzaji wa mazingira. Sayansi na teknolojia asilia
                    zilitumia njia ambazo zilipunguza athari katika mazingira,
                    kukuza uhifadhi wa wanyama na mimea, na kuheshimu
                    uumbaji katika mazingira waliyoishi. Kwa mfano, kwa jamii
                    za wawindaji ilikuwa mwiko kuwinda mnyama ambaye si
                    kwa ajili ya chakula au matumizi ya ngozi yake. Pia, ilikuwa
                    ni mwiko kwa jamii kukata miti ya matunda au ambayo
                    ingetumiwa na wachongaji. Jamii zilikuwa na maarifa ya
                    kutambua miti, mimea na matumizi  yake. Miiko  iliyozuia
                    kukata miti eneo fulani ililenga kuwezesha uwapo wa
                    rasilimali endelevu;

              (f)  Afya ya jamii. Sayansi na teknolojia za asili zilizingatia
                    afya za wengine. Kwa mfano, wachongaji walihakikisha
                    miti waliyotumia kuchongea vyombo vya nyumbani ni



                                                   75




                                                                                          06/11/2024   11:30:10
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   75
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   75                                     06/11/2024   11:30:10
   77   78   79   80   81   82   83   84   85   86   87