Page 78 - Historiayatznamaadili
P. 78

Sayansi na teknolojia za uhifadhi vitu zilifanyika kwa kutumia
              chumvi, moto, moshi, jua au mafuta. Uhifadhi kwa kutumia
              chumvi ulifanyika kwa kupaka au kunyunyiza chumvi kwenye
              nyama na samaki ili kuzihifadhi sizioze. Pia, chumvi ilitumika
              kuhifadhi maiti, ambapo chumvi ilipakwa na kunyunyizwa
          FOR ONLINE READING ONLY
              sehemu mbalimbali za maiti ili kuizuia isiharibike. Sayansi na
              teknolojia ya uhifadhi vitu kwa kutumia jua, ilifanywa kwa kuanika
              vitu juani ili kuvikausha visiharibike. Vitu kama nyama, samaki au

              mboga za majani vilianikwa juani kwa muda mpaka vilipokauka.

              Pia, sayansi na teknolojia ya uhifadhi vitu ilitumia moshi. Moshi
              ulitumika kuhifadhi vitu kama vile nyama, samaki na nafaka,
              ambapo vitu vilibanikwa juu ya kichanja ili vipate moshi. Vilevile,
              moto ulitumika kuhifadhi vitu kama nyama na samaki, kwa lengo

              la kubanika, kuchoma kuchemsha na kukausha ili visioze. Mafuta
              mbalimbali ya asili kama vile mafuta ya minyonyo yalitumika
              kupaka ili kuhifadhia vitu visiharibike.


                      Zoezi namba 4

                Oanisha maneno ya sehemu A na maelezo yaliyopo sehemu
                B kwa kuandika jibu sahihi zaidi sehemu ya jibu.


                    Sehemu A           Jibu                  Sehemu B

                 (i)  Jua                      (a)  kubanika, kuchoma

                 (ii)  Mafuta ya                    kuchemsha na kukausha
                       minyonyo                (b)  kupaka na kunyunyizia

                 (iii)  Moto                   (c)  kupaka

                 (iv)  Chumvi                  (d)  kukausha
                 (v)  Moshi                    (e)  kuanika na kukausha



              Sayansi na teknolojia asilia za uhifadhi hazikuwa na madhara
              kwa binadamu. Uhifadhi haukutumia dawa zenye kemikali kama

              ilivyo sasa, ambapo baadhi zina madhara kwa binadamu.



                                                   71




                                                                                          06/11/2024   11:30:05
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   71                                     06/11/2024   11:30:05
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   71
   73   74   75   76   77   78   79   80   81   82   83