Page 77 - Historiayatznamaadili
P. 77

Pia, chumvi ilipatikana kwa kukausha maji yenye asili ya chumvi
              kwenye jua na mabaki yalizolewa kama chumvi. Jamii zilizotumia
              sayansi na teknolojia hii ya kutengeneza chumvi, zilitengeneza
              matuta yaliyoitwa mabirika maeneo ya bahari au ziwa yenye maji
          FOR ONLINE READING ONLY
              ya asili ya chumvi ili kukinga maji. Maji yaliingia kwenye mabirika
              hayo wakati wa maji kujaa, kisha maji yalikaushwa kwa njia ya
              mvuke wa joto la jua. Mabaki yaliyokauka yalikusanywa kama
              chumvi. Kielelezo namba 25, kinaonesha sayansi na teknolojia

              ya kutengeneza chumvi kwa kukinga maji kwenye “mabirika” na
              kukaushwa kwa jua ili kupata chumvi.































                 Kielelezo namba 25: Sayansi na teknolojia ya kutayarisha chumvi

              Sayansi na teknolojia za asilia katika uhifadhi wa vitu

              Jamii za kale zilikuwa na sayansi na teknolojia mbalimbali za
              kuhifadhi vyakula na nafaka kwa muda fulani ili visiharibike.

                                Kazi ya kufanya namba 13


                           Fanya uchunguzi wa mbinu za asili za uhifadhi wa
                           vitu kama vyakula, nyama, samaki, mazao na maiti
                           katika jamii inayokuzunguka.



                                                   70




                                                                                          06/11/2024   11:30:05
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   70
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   70                                     06/11/2024   11:30:05
   72   73   74   75   76   77   78   79   80   81   82