Page 75 - Historiayatznamaadili
P. 75

mkubwa katika kubaini miti iliyofaa kwa uchongaji na kutengeneza
              chombo kilichokusudiwa. Kwa mfano, miti iliyotumika
              kutengenezea mitumbwi na ngalawa ilikuwa mikubwa na yenye
              sifa ya kutokunyonya maji. Miti iliyotumika kutengenezea vyombo
          FOR ONLINE READING ONLY
              kama sahani, bakuli, miko na upawa ilitakiwa isiwe michungu
              na yenye sumu. Zana zilizotumika kwa uchongaji zilitofautiana
              kulingana na chombo kilichokusudiwa kutengenezwa. Mfano,
              zana zilizotumika kutengenezea vifaa vya nyumbani, vinyago

              na mapambo hazikuwa sawa na zilizotumika kutengenezea
              mitumbwi na ngalawa. Kielelezo namba 23, kinaonesha shughuli
              za uchongaji.
































                      Kielelezo namba 23: Sayansi na teknolojia ya uchongaji

              Baadhi ya jamii zilikuwa na sayansi na teknolojia ya kutengeneza
              mashine mbalimbali. Mfano, jamii za Wahaya zilitengeneza

              mashine za kusaga na kukoboa nafaka. Mashine zilitengenezwa
              kwa kuchonga gogo kubwa na ndani yake viliwekwa vyuma laini
              vilivyopishana ili kuwezesha kusaga kitu. Mashine hizi zilitumika
              kusaga na kukoboa nafaka.





                                                   68




                                                                                          06/11/2024   11:30:03
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   68                                     06/11/2024   11:30:03
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   68
   70   71   72   73   74   75   76   77   78   79   80