Page 93 - Historiayatznamaadili
P. 93

Uhunzi ilikuwa shughuli ya uchumi katika jamii kabla ya ukoloni.
              Shughuli za uhunzi zilifanyika kwa ajili ya kukidhi mahitaji ya
              jamii na biashara. Baadhi ya jamii zilizojishughulisha na uhunzi
              ni Wanyambo, Wahaya, Wazinza, Wafipa, Wapare, na Wayao.
              Shughuli za uhunzi zilifanyika kwa wahunzi kufua chuma, kisha
          FOR ONLINE READING ONLY
              kutengeneza zana mbalimbali za chuma. Mfano, zana za chuma
              zilizotengenezwa ni majembe, mashoka, mundu, mapanga,
              mikuki na mishale.


              Zana hizi zilichangia maendeleo katika shughuli za kilimo, uvuvi
              na uwindaji. Pia, zana hizi zilileta mapinduzi katika silaha za
              ulinzi. Zana za chuma kama vile mikuki na mishale zilitumika
              kujihami dhidi ya maadui na wanyama wakali. Pia, zana hizi
              zilitumika katika uwindaji kwa kuwawezesha wawindaji kupata

              mawindo ya wanyama na kuwa na ziada. Viwanda vya uhunzi
              vilikuwa na mchango mkubwa katika kuendeleza shughuli
              zingine za uchumi katika jamii kabla ya ukoloni.


                                Kazi ya kufanya namba 5

                           Jadili namna ya kuendeleza shughuli za uhunzi
                           nchini kwa sasa ili kukuza uchumi wa viwanda.




              Wahunzi hoyee! Watu wote kwenye hadhara waliitikia hoyee,
              kisha wakapiga makofi na vigelegele. Wageni walifurahi sana
              kusikia kuhusu maendeleo ya shughuli za uhunzi.


                      Zoezi namba 3

                1.  Bainisha maendeleo katika shughuli za uhunzi kabla ya

                      ukoloni.
                2.  Fafanua mchango wa shughuli za uhunzi katika shughuli
                      zingine za uchumi kabla ya ukoloni.


              Mgeni aliyefuata  alikuwa Bibi  Mkisi wa  kabila la  Wakisi

              akiwakilisha jamii za wafinyanzi.


                                                   86




                                                                                          06/11/2024   11:30:12
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   86                                     06/11/2024   11:30:12
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   86
   88   89   90   91   92   93   94   95   96   97   98