Page 94 - Historiayatznamaadili
P. 94
Shughuli za uchumi za ufinyanzi
Bibi Mkisi alianza kuelezea kwa kusema:
Jamii za wafinyanzi zilikuwa na viwanda vya kufinyanga vitu
mbalimbali. Mfano wa vitu hivyo ni vyungu, bakuli, sahani na
FOR ONLINE READING ONLY
birika. Pia, jamii hizi zilitengeneza mitungi, tanuru na vibia.
Vyombo hivi vilitumika kwa
ajili ya matumizi mbalimbali
kama vile kupikia, kuhifadhi
maji, kuteka maji na kulia
chakula. Jamii za wafinyanzi
zilitengeneza vyombo imara
kabla ya kuja kwa wakoloni.
Mnaona vyombo hivi? Bibi
Nyamasi alionesha baadhi
ya vyombo vya mfinyanzi
walivyotengeneza kama
inavyoonekana katika Kielelezo namba 3: Vyombo vya
kielelezo namba 3. ufinyanzi
Vyombo hivi vilifinyangwa kwa kutumia udongo wa mfinyanzi.
Jamii nyingi kwa sasa zinafanya shughuli za uchumi za ufinyanzi.
Awali, jamii zilizokuwa maarufu kwa shughuli za ufinyanzi
ni Wakisi kutoka Kaskazini mwa ziwa Nyasa. Hali kadhalika
Wapare kutoka Kilimanjaro na Wafipa kutoka Sumbawanga
walikuwa maarufu kwa kazi za ufinyanzi. Vyungu vya Wakisi
vilikuwa imara zaidi na havikuvunjika hovyo hovyo kwa sababu
vilifinyangwa kwa udongo mzuri zaidi na vilikaushwa kivulini.
Ufinyanzi ilikuwa shughuli kuu ya uchumi kwa jamii za wafinyanzi.
Shughuli za ufinyanzi zilifanyika kwa ajili ya kukidhi mahitaji
ya jamii na biashara. Biashara zilifanyika ili kupata bidhaa
zilizokosekana katika jamii za wafinyanzi. Hii ilisaidia kuleta
maendeleo katika jamii za wafinyanzi.
87
06/11/2024 11:30:13
Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd 87 06/11/2024 11:30:13
Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd 87