Page 96 - Historiayatznamaadili
P. 96

za Wanyiha, Wandali, Wajita, Wahehe, Wahaya Wazaramo
              na Wanyamwanga walikuwa maarufu kwa usukaji. Jamii hizi
              zilibadilishana bidhaa za ususi na jamii zingine ili kupata bidhaa
              ambazo hazikuwapo katika jamii zao.
          FOR ONLINE READING ONLY
              Mzee Pakawa alimaliza simulizi na wageni walishangilia kwa
              vifijo.

                                Kazi ya kufanya namba 7


                           Fanya uchunguzi kwa kuuliza, kusoma matini au
                           kutembelea maeneo yenye shughuli za ususi na
                           kisha eleza namna ya kuziendeleza shughuli hizo
                           kwa matumizi ya sasa.



              Shughuli za uchumi za uchongaji

              Alifuata Mzee Kukawa kutoka jamii za Wamakonde.  Yeye
              aliwakilisha shughuli za uchumi katika viwanda vya wachongaji.
              Mzee Kukawa alianza simulizi kwa kuelezea wageni kuwa:

              Uchongaji ulikuwa ni shughuli kuu ya uchumi katika jamii
              mbalimbali kabla ya ukoloni. Shughuli za uchongaji zilifanywa
              kwa kuchonga vyombo vya chakula kama bakuli, sahani na

              vijiko. Pia, jamii zilichonga vinu, michi, vigoda, marimba, chanuo,
              pawa, vibakuli, miko na viti. Mzee Kukawa alionesha vyombo
              vya kuchonga katika Kielelezo namba 5.




















                             Kielelezo namba 5:  Vyombo vya kuchonga


                                                   89




                                                                                          06/11/2024   11:30:13
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   89
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   89                                     06/11/2024   11:30:13
   91   92   93   94   95   96   97   98   99   100   101