Page 101 - Historiayatznamaadili
P. 101

kuwa mahitaji yote ya shughuli za uchumi yalitokana na rasilimali
              asilia katika mazingira yao. Jamii zilitambua kuwa rasilimali asili
              ndizo zilizowapatia chakula, dawa (mizizi, majani na magome ya
              miti) na malighafi kwa ajili ya shughuli za uchumi. Pia, rasilimali
              asilia zilikuwa chanzo cha mvua. Hivyo, jamii ziliweka kanuni na
          FOR ONLINE READING ONLY
              taratibu za kimaadili katika ulinzi na matumizi ya rasilimali asilia
              ili kuongeza ufanisi katika utendekaji wa shughuli za uchumi.
              Aidha, maadili yaliendana na aina ya shughuli ya uchumi,
              mazingira ya kijiografia na malighafi zilizotumika.


              Maadili katika ulinzi wa rasilimali asilia

              Miiko ilitumika kama sehemu ya maadili  ili kulinda  rasilimali
              adimu zilizotumika kwa ajili  ya uchumi. Miiko ilikataza watu
              kukata aina fulani za miti, watu kulima katika vyanzo vya maji
              kama vile, mito na maziwa. Pia, ilikataza kulima maeneo fulani
              ya ardhi. Uhifadhi wa ardhi na misitu uliambatana na sheria za
              mila zilizozuia kukata miti kiholela ili kupunguza uharibifu wa
              misitu na kuhifadhi rasilimali asilia.

              Jamii za wavuvi ziliweka taratibu za kipindi cha kuvua, maeneo
              ya kuvua, na aina za samaki za kuvuliwa ili kuruhusu samaki

              kuzaliana na kukua. Pia, ulinzi ulifanyika mazingira ya maji,
              ili kuzuia uvuvi wa kupita kiasi na kuvua samaki wachanga.
              Jamii za wakulima zilichoma vichaka katika eneo la shamba
              jipya ili kuondoa uchafu na wadudu waharibifu. Pia, zilifanya
              kilimo cha mseto ambapo mazao tofauti yalipandwa pamoja ili
              kuongeza uzalishaji na kudumisha rutuba ya ardhi. Desturi hizi
              ziliwasaidia kupunguza magonjwa ya mimea na hivyo kuongeza
              mazao ya kilimo. Vilevile, mimea maalumu ilitumika kama dawa
              katika kuzuia magonjwa na kuua wadudu katika mimea, ili kuzuia
              athari za sumu kwa binadamu katika mazao. Aidha, wakulima
              walichagua mazao bora na kuyahifadhi kama mbegu kwa ajili
              ya msimu wa kilimo unaofuata. Maadili haya yalisaidia kulinda

              afya ya jamii na kuhifadhi maeneo yenye rasilimali adimu kwa
              shughuli za uchumi katika jamii, kwa faida ya jamii zao na vizazi
              vijavyo.



                                                   94




                                                                                          06/11/2024   11:30:15
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   94                                     06/11/2024   11:30:15
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   94
   96   97   98   99   100   101   102   103   104   105   106