Page 102 - Historiayatznamaadili
P. 102

Kimsingi, miiko hii ililenga kulinda uharibifu wa vyanzo vya
              uchumi kama vile aina ya miti iliyotumika katika ujenzi, uchongaji
              na dawa. Pia, ililenga kutunza vyanzo vya maji na rasilimali
              zilizopo majini na kuhifadhi ardhi kwa matumizi ya baadaye.
          FOR ONLINE READING ONLY
                      Zoezi namba 5


                1.  Bainisha maadili yaliyozingatiwa katika uvuvi ili kulinda

                      rasilimali za uvuvi kabla ya ukoloni.
                2.  Eleza umuhimu wa maadili katika uvuvi katika kuendeleza

                      uvuvi kabla ya ukoloni.
                3.  Eleza umuhimu wa maadili ya kilimo katika kuendeleza
                      kilimo kabla ya ukoloni.



              Maadili katika kutunza afya ya jamii

              Miiko iliwekwa ya kukataza kufanya shughuli za uhunzi maeneo

              ya karibu na makazi ya watu. Hivyo, chuma kilifuliwa maeneo
              ya misituni na katika matanuru yaliyosaidia kuongeza nguvu ya
              joto na kupunguza moshi mkali utokanao na kazi ya kuyeyusha
              chuma. Pia, wanawake wajawazito walizuiwa kuwa karibu na

              maeneo yenye shughuli za uhunzi ili kuzuia athari za joto na moshi
              mkali uliotoka katika tanuru kwa afya ya mama na mtoto. Vivyo
              hivyo, shughuli zilizosababisha kuharibu mazalia ya samaki na
              kuchafua vyanzo vya maji zilizuiliwa. Vilevile, palikuwapo na miti

              maalumu iliyotumika katika shughuli za uchongaji. Hii ilisaidia
              kuondoa matumizi ya miti ambayo ingeleta madhara kwa afya ya
              binadamu. Wavuvi walitumia mbinu za uvuvi zilizolinda mazao ya
              uvuvi. Mfano, walitumia mimea yenye kulevya samaki ili kuwavua

              na siyo iliyoua samaki. Matumizi ya mbegu zilizohifadhiwa kwa
              njia asilia katika kilimo yalisaidia kulinda afya ya jamii dhidi ya
              magonjwa yatokanayo na sumu za mimea.







                                                   95




                                                                                          06/11/2024   11:30:15
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   95
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   95                                     06/11/2024   11:30:15
   97   98   99   100   101   102   103   104   105   106   107