Page 104 - Historiayatznamaadili
P. 104

walifanya kazi pamoja kwa lengo la kusaidiana na kuongeza
              ufanisi katika shughuli husika. Mfano, jamii zilisaidiana katika
              shughuli kama vile kupanda, kuvuna, kuhifadhi mazao, uhunzi,
              ufinyanzi, uvuvi na kadhalika. Hii ilisaidia kuongeza ufanisi katika
          FOR ONLINE READING ONLY
              kazi na kukuza uhusiano katika jamii husika. Aidha, jamii zilimiliki
              shughuli za uchumi pamoja. Viongozi wa familia, ukoo au jamii
              walikuwa wadhamini tu katika kusimamia shughuli za uchumi.


              Watu wenye ujuzi, stadi na maarifa ya kufanya shughuli za
              uchumi waliwafundisha vijana ili kurithisha maarifa na ujuzi
              mahususi. Pia, shughuli za uchumi katika jamii zilifanyika kwa

              siri kubwa ili kuhifadhi maarifa na ujuzi katika shughuli za uchumi
              kwa jamii husika. Hii ilisaidia kuhifadhi maarifa na kuimarisha
              utamaduni wa shughuli za uchumi kutoka kizazi kimoja hadi
              kingine.

                      Zoezi namba 7

                1.  Ainisha maadili yaliyozingatiwa katika utendaji wa kazi

                      katika shughuli za uchumi.
                2.  Fafanua umuhimu wa maadili katika utendaji wa kazi

                      katika shughuli za uchumi.



                                Kazi ya kufanya namba 12

                           Jadili mambo uliyojifunza kuhusu maadili katika
                           shughuli  za  uchumi,  kisha  andaa  mpango  wa

                           kuyaendeleza katika jamii ya sasa.



              Wajibu wa jamii katika kuendeleza shughuli za uchumi

              Jamii ya sasa inao wajibu wa kupenda na kuthamini shughuli
              za jamii zilizofanyika awali.  Kila mwanajamii anao wajibu wa
              kuzitambua shughuli za uchumi za kabla ya ukoloni na kufanya

              kazi ili kuziendeleza katika jamii yake. Aidha, jamii inapaswa



                                                   97




                                                                                          06/11/2024   11:30:15
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   97                                     06/11/2024   11:30:15
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   97
   99   100   101   102   103   104   105   106   107   108   109