Page 109 - Historiayatznamaadili
P. 109

Zoezi namba 1


                1.  Eleza mambo uliyojifunza katika kujenga ushirikiano na
                      uhusiano mwema.
          FOR ONLINE READING ONLY
                2.  Eleza jinsi misingi ya utu, heshima, upendo, ukweli,
                      uaminifu na amani inavyokuza na kutunza ushirikiano
                      na uhusiano.


              Ushirikiano na uhusiano wa kijamii

              Ushirikiano na uhusiano wa kijamii ulijengwa kwa kushirikiana
              na kuhusiana katika shughuli za kijamii.


                                Kazi ya kufanya namba 4

                           Waulize wazazi au walezi kuhusu namna jamii za
                           kale zilivyojenga ushirikiano na uhusiano wa kijamii.





              Ushirikiano na uhusiano kijamii katika misingi ya ujima

              Ushirikiano na uhusiano katika jamii za awali kabisa ulikuzwa
              katika misingi ya ujima. Ujima ni mfumo wa awali kabisa wa
              kijamii, kiutawala na kiuchumi katika maendeleo ya binadamu.

              Katika kipindi cha ujima watu wote walimiliki rasilimali kwa
              pamoja na walifanya kazi pamoja. Kwa mfano, jamii zilishirikiana
              katika shughuli kama vile kilimo, uvuvi, uwindaji na kadhalika.
              Shughuli za kilimo na uvuvi katika kipindi cha ujima zilikuwa bado

              ni za chini kutokana na ukosefu wa zana imara za uzalishaji
              mali katika jamii. Zana zilizotumika katika kipindi hiki zilikuwa
              zana za mawe.  Mawe yalitumika kutengeneza zana kama vile
              mikuki, mishale, mashoka, visu na kadhalika. Baadhi ya zana

              hizi ziliwekwa mpini ili kurahisisha matumizi yake. Zana hizi za
              mawe zilitumika katika kazi za uwindaji, kulima, kuchimba mizizi
              na kusaga nafaka mbalimbali. Kielelezo namba 1, kinaonesha
              binadamu aliyebeba zana za mawe zilizowekwa mpini.



                                                   102




                                                                                          06/11/2024   11:30:17
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   102
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   102                                    06/11/2024   11:30:17
   104   105   106   107   108   109   110   111   112   113   114