Page 105 - Historiayatznamaadili
P. 105

kutambua misingi ya utendekaji wa kazi na maadili yake na
              kuiendeleza katika jamii ya sasa.


              Mapinduzi ya sayansi na teknolojia yatumike sambamba na
              uendelezaji wa shughuli za uchumi kwa sasa ili kuleta maendeleo
          FOR ONLINE READING ONLY
              zaidi. Aidha, viongozi wa familia, ukoo au jamii wanapaswa
              kusimamia shughuli za uchumi ili kuleta maendeleo kuanzia
              ngazi ya chini kwa matumizi ya sasa na baadaye. Pia, usimamizi

              huu utasaidia kuongeza ubunifu na ukuzaji wa viwanda na
              kuongeza mianya ya ajira.


                                Kazi ya kufanya namba 13


                           Jadili na andaa mikakati ya kufuatilia uendelezaji wa
                           shughuli za uchumi katika jamii yako.






                        Zoezi la jumla

               1.  Taja maendeleo yaliyofikiwa na jamii katika shughuli za
                     kilimo kabla ya ukoloni.

               2.  Toa mifano ya viashirio vya maendeleo kwa jamii kabla
                     ya kuingia kwa ukoloni.

               3.  Taja faida ya shughuli za uchumi katika jamii kabla ya
                     ukoloni.

               4.  Bainisha maadili yaliyosisitizwa katika shughuli za uchumi
                     kabla ya ukoloni.

               5.  Je, kuna umuhimu gani wa kuendeleza maadili katika
                     shughuli za uchumi kabla ya ukoloni kwa sasa?

               6.  Eleza mambo ya kujifunza kutokana na shughuli za
                     uchumi kabla ya ukoloni.








                                                   98




                                                                                          06/11/2024   11:30:16
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   98
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   98                                     06/11/2024   11:30:16
   100   101   102   103   104   105   106   107   108   109   110