Page 108 - Historiayatznamaadili
P. 108

familia na familia, jamii na jamii au Taifa na Taifa lingine.
              Pia, ushirikiano huelezea namna watu wanavyofanya kazi au
              shughuli fulani kwa pamoja. Kadiri watu wanavyoshirikiana,
              ndivyo wanavyojenga uhusiano.
          FOR ONLINE READING ONLY
                                Kazi ya kufanya namba 2

                             Andika mambo ya kuzingatia katika kujenga
                             ushirikiano na uhusiano mwema.




              Ushirikiano na uhusiano hujengwa kwa misingi ya utu, upendo,
              ukweli, uaminifu, amani na heshima. Pia, hujengwa kwa kuwa
              na mawasiliano mazuri, kutembeleana mara kwa mara, kufanya
              kazi  kwa  pamoja,  kuepuka  dhuluma  na  kujenga  tabia  ya

              kuheshimu mipaka ya watu wengine. Watu wakiwa na uhusiano
              mwema husaidiana, hupendana na huheshimiana. Ushirikiano
              na uhusiano mwema haubagui jinsi, kabila, umri, dini wala
              rangi. Ushirikiano na uhusiano mwema huleta mafanikio katika

              maisha. Kwa hiyo, ni vizuri kujenga uhusiano mwema na watu
              wanaotuzunguka katika maisha yetu ya kila siku.

                                Kazi ya kufanya namba 3


                           Andika maana ya maneno utu, heshima, upendo,
                           ukweli, uaminifu na amani.




              Tangu kale, jamii zilikuwa na ushirikiano na uhusiano kati yao
              na jamii zingine. Ushirikiano na uhusiano huo ulijengwa katika
              misingi ya utu, upendo, heshima, amani na ukweli. Jamii ziliepuka
              dhuluma na ziliheshimu mipaka ya watu wengine. Hii ilisaidia
              kujenga uaminifu katika jamii na kukuza uhusiano. Hapakuwa na

              ubaguzi wala matabaka. Aidha, aina za ushirikiano na uhusiano
              zilitofautiana na nyakati kulingana na maendeleo ya sayansi na
              teknolojia.




                                                   101




                                                                                          06/11/2024   11:30:16
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   101                                    06/11/2024   11:30:16
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   101
   103   104   105   106   107   108   109   110   111   112   113