Page 112 - Historiayatznamaadili
P. 112

Msingi wa mfumo huu wa uhusiano ulikuwa umiliki wa ardhi.
              Mfumo huu ulienea maeneo yenye wakulima wakubwa, ambao
              walimiliki ardhi na kuikodisha kwa watu wasio na ardhi katika

              maeneo yao. Mfano wa mfumo huu ni  Nyarubanja, katika
          FOR ONLINE READING ONLY
              jamii za Wahaya. Mfumo wa Nyarubanja ulihusisha tabaka la

              Abatwazi ambao ni walimiliki wa ardhi na Abatwana ambao
              walipewa ardhi na kufanya kazi kwenye maeneo ya Abatwazi.
              Abatwana walilima na kuleta sehemu ya mazao kwa Abatwazi.

              Pia, mfumo huu ulikuwapo maeneo ya jamii za Pwani ya Bahari
              ya Hindi na ulijulikana kama  Umwinyi Mkuu.  Mwinyi Mkuu
              alimiliki ardhi, mifugo  na  watwana. Watwana hawakumiliki

              ardhi na hawakuruhusiwa kabisa kumiliki rasilimali katika jamii.
              Hivyo, walikodi ardhi au mifugo kutoka kwa watawala ambao ni
              “mamwinyi” na kurudisha sehemu ya mazao kwa Mwinyi kama

              ushuru.


              Mfumo wa ukabaila ndio ulioanzisha mizizi ya unyonyaji na
              ubaguzi katika ushirikiano na uhusiano katika jamii za kale.
              Misingi ya utu, upendo, usawa na amani ilianza kuondoka katika

              ushirikiano na uhusiano wa jamii. Dhuluma na ubaguzi vilianza
              kukua katika jamii. Jamii zingine zilizokuwa na mfumo huu ni
              jamii ya Waha, Wapare, Wachaga, Wahangaza na Wanyambo.

              Maeneo  haya  yote  yalikuwa  imara  katika  kilimo  na  ufugaji
              kutokana na ugunduzi wa chuma.



                                Kazi ya kufanya namba 5



                           Jadili tofauti zilizokuwapo kati ya mfumo wa ujima
                           na ukabaila.










                                                   105




                                                                                          06/11/2024   11:30:17
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   105                                    06/11/2024   11:30:17
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   105
   107   108   109   110   111   112   113   114   115   116   117