Page 115 - Historiayatznamaadili
P. 115

ya masafa marefu ilianza baada ya watu kuona haja ya kwenda
              maeneo ya mbali zaidi ili kupata bidhaa ambazo jamii hazikuweza
              kuzipata kutoka katika jamii za karibu. Mwanzoni biashara hii

              ilihusisha jamii za wahunzi, wakulima, wasusi, wachongaji na
          FOR ONLINE READING ONLY
              wafinyanzi. Biashara hii baadaye ilikua zaidi na hata kuhusisha

              jamii kutoka nje ya mipaka ya nchi yetu. Biashara hii ilifanyika
              maeneo ya Kaskazini, Kusini, Kusini Magharibi, Magharibi na
              Kaskazini Magharibi mwa nchi ya Tanzania.


              Ukanda wa Kaskazini mwa Tanzania; jamii zilizohusiana na
              kushirikiana kibiashara ni Wapare, Wachaga, Wasambaa na

              Wamasai. Wapare walikuwa maarufu katika biashara ya ukanda
              wa Kaskazini. Hii ilitokana na umaarufu wa jamii ya Wapare katika

              kutengeneza zana za chuma. Pia, jamii hii ilikuwa ya wafinyanzi
              hodari wa vyungu. Hivyo, jamii hii ilibadilishana bidhaa zao na
              Wachaga na Wasambaa. Kutoka kwa Wachaga walipata ndizi

              na mazao mengine ya chakula. Wamasai walibadilishana na
              Wapare mifugo ili wapate zana za chuma kama vile mikuki na
              sime zilizotumika katika kulinda mifugo. Ushirikiano na uhusiano

              wa biashara ya jamii hizi ulikwenda hadi kwa jamii za Wakamba
              na Wataita walioishi Kenya.


              Katika ukanda wa Kusini, uhusiano wa ushirikiano wa biashara
              ulifanyika kati ya watu wa Pwani ya Msumbiji na ya Tanzania.

              Biashara  hii  ilimilikiwa  zaidi na jamii ya Wayao. Wayao
              walibadilishana bidhaa kama majembe, tumbaku na vyungu na

              jamii za Pwani ili kupata chumvi na mazao ya chakula. Biashara
              hii ilivuka mipaka ya Tanzania hadi Malawi, Zambia na Angola.
              Bidhaa muhimu baina ya nchi hizi na Wayao zilikuwa chumvi na

              zana za chuma na shaba.

              Upande wa Kusini Magharibi mwa Tanzania, jamii zilizohusiana

              na kushirikiana kibiashara ni Wanyakyusa, Wakinga, Wakisi na


                                                   108




                                                                                          06/11/2024   11:30:18
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   108
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   108                                    06/11/2024   11:30:18
   110   111   112   113   114   115   116   117   118   119   120