Page 118 - Historiayatznamaadili
P. 118

Baadaye, hasa kipindi cha karne ya 19, biashara hii ilihusisha
              biashara ya utumwa na pembe za ndovu. Kielelezo namba
              4, kinaonesha bidhaa za pembe za ndovu walizochukua
              wafanyabiashara wakati huo.
          FOR ONLINE READING ONLY




























                                Kielelezo namba 4:  Pembe za ndovu

              Pembe za ndovu zilitoka sehemu za mikoa yenye mbuga za
              wanyama na  kupelekwa  Pwani  ya  Bahari ya Hindi.  Vilevile,
              wafanyabiashara hawa walichukua watumwa wachache kutoka
              Pwani ya Bahari ya Hindi na kuwasafirisha kwenda nchi za

              Mashariki ya Kati. Kutoka Mashariki ya Mbali na Kati,
              wafanyabiashara hao walileta bidhaa kama vile nguo, shanga,
              vyombo vya kauri na visu. Biashara hii ndiyo iliyosababisha kukua
              kwa miji ya Bagamoyo, Kilwa Kivinje na Zanzibar.


                      Zoezi namba 4

                1.  Eleza mambo uliyojifunza kuhusu biashara ya masafa

                      marefu.
                2.  Eleza  jinsi  jamii  za  sasa  zinavyoweza  kuimarisha
                      biashara kwa kutumia stadi ulizojifunza.





                                                   111




                                                                                          06/11/2024   11:30:19
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   111
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   111                                    06/11/2024   11:30:19
   113   114   115   116   117   118   119   120   121   122   123