Page 120 - Historiayatznamaadili
P. 120

Wapare walizalisha zana za chuma kwa wingi. Kadhalika jamii
              za wachongaji, wafinyanzi na wasusi zilizalisha bidhaa zao
              zaidi. Jamii hizo zilijishughulisha zaidi na shughuli za uchumi ili
              kuendana na mahitaji katika biashara. Kimsingi, ushirikiano na
              uhusiano wa kibiashara ulichangia kuendelea kwa shughuli za
          FOR ONLINE READING ONLY
              uchumi katika viwanda kama vile, ufinyanzi, uhunzi, uchongaji,
              ususi na shughuli za kilimo kabla ya ukoloni.


              Uhitaji wa bidhaa kwa ajili ya biashara ulisababisha kuibuka
              kwa watu maalumu ambao kazi yao kubwa ilikuwa kufanya
              biashara. Pia, biashara zilisababisha jamii kujifunza ujuzi na
              stadi za jamii zingine. Jamii ziliiga stadi  za  jamii  nyingine  kwa
              kuona  na  kutumia  bidhaa  za jamii zingine. Vilevile, uhusiano
              wa kibiashara kati ya wafanyabiashara wa masafa marefu na

              jamii za Mashariki ya Kati na Pwani ya Afrika Mashariki ulichangia
              kuenea na kukua kwa lugha ya Kiswahili. Lugha hii ilikuwa
              kama hitaji la biashara ili watu kuweza kuwasiliana. Licha ya
              kukuza lugha ya Kiswahili, biashara hii ndiyo iliyoeneza dini na
              utamaduni wa Kiislamu kama vile uvaaji wa kanzu na baibui hasa
              maeneo ya miji ya Pwani ya Bahari ya Hindi na maeneo ya Ujiji
              na Tabora. Hii ilitokana na wafanyabiashara kutoka Tabora na

              Ujiji kushirikiana na wafanyabiashara hawa, haswa wakati wa
              biashara ya utumwa.

                                Kazi ya kufanya namba 7

                           Fanya mdahalo kuhusu mada “jamii za Kitanzania

                           hazikuwa  na  maendeleo,  ujio  wa  wakoloni  ndio
                           ulioleta maendeleo ya kiuchumi na kijamii nchini”.


              Jamii zilikuwa na maendeleo ya kijamii na kiuchumi kabla ya kuja

              kwa ukoloni nchini. Ukoloni haukuwa chanzo cha maendeleo
              ya kiuchumi na ya kijamii nchini. Ukoloni ulileta mabadiliko ya
              mfumo wa maisha nchini na sio mwanzo wa maendeleo nchini.







                                                   113




                                                                                          06/11/2024   11:30:19
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   113                                    06/11/2024   11:30:19
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   113
   115   116   117   118   119   120   121   122   123   124   125