Page 119 - Historiayatznamaadili
P. 119

Kazi ya kufanya namba 6

                           Soma matini mbalimbali na maktaba mtandao kuhusu

                           mchango wa biashara ya masafa marefu katika
                           kukua kwa biashara ya wageni kutoka Mashariki ya
          FOR ONLINE READING ONLY
                           Mbali na Kati kabla ya ukoloni.



              Mchango wa uhusiano wa biashara katika uchumi na jamii
              Ushirikiano na uhusiano wa biashara baina ya jamii na jamii na

              ile ya masafa marefu ulileta maendeleo katika jamii zetu. Jamii
              zilitumia bidhaa walizobadilishana kuimarisha jamii zao. Mfano,
              jamii zilitumia silaha walizozipata kutoka kwa wahunzi kuimarisha
              mfumo wa ulinzi katika jamii zao. Pia, biashara hizi zilisababisha
              kukua kwa mamlaka za utawala wa jadi. Hii ni kutokana na

              umiliki wa njia za biashara. Mfano wa mamlaka hizo ni tawala
              za  Wanyamwezi (Mtemi Isike na Mirambo) Wahehe (Mutwa
              Mkwawa), Wayao (Chifu Machemba) na Wahaya (Omukama

              Rumanyika). Viongozi wa jamii hizo walikusanya ushuru kutoka
              kwa wafanyabiashara waliopita maeneo yao. Vilevile, tawala za
              Umwinyi zilikua zaidi kutokana na uhusiano wa kibiashara haswa
              na wageni kutoka Mashariki ya Kati.


              Biashara hizi pia zilisababisha kukua kwa miji ya kifahari. Maeneo
              ambapo biashara zilifanyika palijengwa majumba makubwa ya
              mawe pamoja na misikiti na majumba ya kisultani. Maeneo hayo

              ni Kilwa, Bagamoyo na Zanzibar. Miji ya Ujiji na Tabora ilikua
              kutokana na biashara hii.


              Biashara hizi, licha ya kuleta maendeleo ya kijamii, zilisababisha
              kukua kwa shughuli za uchumi. Watu walizalisha bidhaa siyo
              kwa lengo la kujikimu tu, bali kupata ziada kwa ajili ya biashara.
              Hii ilisababisha kuwapo kwa  watu  ambao  walizalisha  bidhaa

              kwa ajili ya biashara. Mfano, Uvinza ilianzisha kikundi ambacho
              kazi yao kubwa ilikuwa kuzalisha chumvi. Wahaya, Wafipa na



                                                   112




                                                                                          06/11/2024   11:30:19
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   112
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   112                                    06/11/2024   11:30:19
   114   115   116   117   118   119   120   121   122   123   124