Page 124 - Historiayatznamaadili
P. 124

kitemi zilijishughulisha na kilimo cha msimu na ufugaji. Shughuli
              za ufugaji na kilimo zilihitaji kuongeza maeneo zaidi ili kukidhi
              mahitaji ya jamii zao. Hivyo, viongozi wa jamii za “Watemi”
              walifanya uvamizi katika jamii zingine ili kujenga utawala wao.
          FOR ONLINE READING ONLY
              Mambo yaliyosababisha kukua kwa tawala za Watemi

              Shughuli za kilimo na ufugaji zilikuwa na mchango mkubwa
              katika kukua kwa utawala wa Watemi. Aidha, ugunduzi wa
              chuma, uliosababisha upatikanaji wa zana kama vile, mashoka,
              visu, mapanga, majembe, mundu, mishale na mikuki ulisaidia
              zaidi tawala hizi kuimarika. Zana hizo ziliimarisha zaidi shughuli
              za kilimo na ufugaji.  Hivyo, kuongezeka kwa uzalishaji katika

              jamii na kuwa na ziada. Pia, ugunduzi wa chuma ulizisaidia
              mamlaka za jadi kupata zana kama vile mikuki, mishale na
              pinde zilizotumika kama silaha za vita katika uvamizi wa jamii
              zilizowazunguka na kuweza kumiliki maeneo makubwa zaidi.

              Vilevile, ukuaji wa jamii za Kitemi ulichangiwa na ushiriki katika

              biashara za jamii na zile za masafa marefu. Jamii za Kitemi
              zilishiriki biashara hizi na kupata bidhaa mbalimbali zilizosaidia
              kukua  kwa  mamlaka  zao.  Aidha,  ujio  wa  wafanyabiashara
              kutoka Mashariki ya Mbali na Kati katika Pwani ya Bahari ya
              Hindi kulichangia zaidi kukua kwa mamlaka za Watemi nchini.
              Wafanyabiashara hawa walikuta wafanyabiashara wa jamii za
              Kitemi wakifanya biashara toka ndani ya nchi hadi Pwani ya
              Bahari ya Hindi. Hivyo, ukawa mwanzo wa wafanyabiashara
              wa kigeni kuanza kufanya biashara na jamii  za Watemi.

              Biashara hizi ziliwezesha jamii za Kitemi kupata silaha kama
              vile bunduki na vitu vingine mfano nguo, shanga na visu kutoka
              kwa wafanyabiashara hao. Wafanyabiashara hawa wa kigeni,
              hasa Waarabu, walipata malighafi kama vile pembe za ndovu,
              vipusa, ngozi za wanyama na watumwa kutoka kwa wenyeji.
              Bidhaa hizi zilichangia kukua kwa mamlaka za Kitemi. Kwa
              mfano, silaha kama vile visu na bunduki zilitumika kuimarisha

              majeshi ya watawala wa Watemi.



                                                   117




                                                                                          06/11/2024   11:30:20
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   117                                    06/11/2024   11:30:20
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   117
   119   120   121   122   123   124   125   126   127   128   129