Page 126 - Historiayatznamaadili
P. 126

Biashara ziliongeza ushujaa wa kivita kwa himaya ya Mtemi
              Mirambo, kutokana na silaha kama vile bunduki ambazo walizipata
              kutoka kwa wafanyabiashara kutoka Mashariki ya Kati. Mtemi
              Mirambo alibadilishana pembe za ndovu na watumwa ili kupata
              silaha. Pembe za ndovu zilipatikana kutokana na uwindaji wa
          FOR ONLINE READING ONLY
              tembo katika maeneo ya misitu. Watumwa walikuwa mateka wa
              vita alivyopigana na jamii zingine wakati wa upanuzi wa himaya
              yake.  Mtemi Mirambo licha ya kufaidika na bidhaa za biashara,

              pia alitoza ushuru kutoka kwa wafanyabiashara waliopita katika
              himaya yake.  Mtemi Mirambo alimiliki njia ya kati ya biashara ya
              masafa marefu iliyoshirikisha wafanyabiashara kutoka Kongo,
              Burundi, Rwanda na Buganda. (Rejea Kielelezo namba 3, katika
              sura ya Tano). Ushuru uliopatikana kutoka kwa wafanyabiashara
              ulichangia kukua na kuimarika kwa mamlaka ya Mtemi Mirambo.


              Vilevile, jeshi la Mirambo lililojulikana kama “warugaruga”,
              lilisaidia zaidi kuimarisha utawala wa Mtemi Mirambo. Jeshi hili
              lilikuwa na nguvu kubwa kutokana na kuwa na silaha imara na
              mbinu za kivita. Mtemi Mirambo alikuwa na nguvu kubwa za

              kivita na aliweza kupinga wakoloni kuingia katika himaya yake.
              Hii ilitokana na uwezo mkubwa wa kivita na utawala aliokuwa
              nao. Hii ilisababisha wakoloni kumpa jina la “Napoleon wa
              Afrika”, kutokana na uimara wake katika jeshi na vita.


                                Kazi ya kufanya namba 4

                           Jadili mambo uliyojifunza kuhusu utawala wa Mtemi

                           Mirambo na namna ya kuyaendeleza katika utawala
                           wa sasa.



              Mtemi Isike

              Mtemi  Isike  (1858-1893)  alikuwa  kiongozi wa  jamii  za
              Wanyamwezi katika himaya ya Unyanyembe. Kiongozi huyu
              alikuwa na utawala imara na nguvu kubwa ya kijeshi.





                                                   119




                                                                                          06/11/2024   11:30:20
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   119                                    06/11/2024   11:30:20
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   119
   121   122   123   124   125   126   127   128   129   130   131