Page 130 - Historiayatznamaadili
P. 130

Kazi ya kufanya namba 6

                           Soma matini kutoka vyanzo mbalimbali ikiwamo

                           maktaba mtandao kuhusu mfumo wa uongozi ulipo
                           sasa nchini, kisha eleza mambo yanayofanana
          FOR ONLINE READING ONLY
                           na kutofautiana na mfumo wa uongozi wa Mutwa
                           Mkwawa.



              Vilevile, utawala huu ulikua kutokana na shughuli za biashara za

              jamii na jamii na zile za masafa marefu. Kama ilivyokuwa kwa
              watawala wengine, Mutwa Mkwawa alikusanya ushuru kutoka
              kwa wafanyabiashara waliopita katika himaya yake kuelekea
              Pwani ya Bahari ya Hindi kufanya biashara. Ushuru aliokusanya

              ulisaidia kuimarisha utawala wake. Aidha, silaha zilizopatikana
              ziliimarisha na kupanua zaidi himaya yake.

              Mamlaka ya Mutwa Mkwawa ilikuwa ni imara nchini hata kabla ya

              kuja kwa wakoloni. Kama ilivyokuwa desturi ya jamii hii kupinga
              uvamizi na kulinda himaya yao, Mutwa Mkwawa hakuwa tayari
              kuruhusu uvamizi wa wageni katika eneo lake. Mtemi Mkwawa

              aliongoza watu wa jamii yake chini ya jeshi lake imara kupinga
              uvamizi wa Wajerumani katika himaya yake. Mfano, mwaka
              1891 Mtemi Mkwawa aliongoza jeshi lake na kuangamiza zaidi
              ya askari 300 wa jeshi la Wajerumani, pamoja na kamanda wa
              jeshi hilo Emil Von Zelewiski. Uimara wa jeshi la Mtemi Mkwawa

              ulizuia utawala wa Wajerumani kuingia kwenye himaya yake
              kwa zaidi ya miaka minne.


                                Kazi ya kufanya namba 7

                           Jadili mambo uliyojifunza kuhusu utawala wa Mutwa
                           Mkwawa na namna ya kuyaendeleza katika utawala
                           wa sasa.







                                                   123




                                                                                          06/11/2024   11:30:21
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   123                                    06/11/2024   11:30:21
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   123
   125   126   127   128   129   130   131   132   133   134   135