Page 132 - Historiayatznamaadili
P. 132

hazikupatikana katika maeneo yao. Kimsingi, utengenezaji wa
              zana za chuma ulisababisha kustawi kwa biashara katika eneo
              la maziwa makuu. Hii ilitokana na utawala wa Kifalme kujihusisha
              katika biashara na jamii za jirani. Biashara hii kwa kiwango kikubwa
          FOR ONLINE READING ONLY
              ilisababisha dola hizi za Kifalme kuwa imara na zenye nguvu.

              Ujio wa Waarabu katika biashara za masafa marefu, ulikuta
              tawala za Kifalme zinamiliki biashara. Wafalme ndio waliokuwa

              kiunganishi cha wafanyabiashara toka bara na Pwani ya Bahari
              ya Hindi. (Rejea kielelezo namba 3, sura ya 5). Umiliki wa
              biashara ulisaidia kukua kwa himaya za Wafalme.  Hii ilitokana

              na ushuru walioutoza kwa kila mfanyabiashara aliyepita maeneo
              ya falme hizi. Wafanyabiashara walilazimika kulipa kodi, mazao
              na vito vya thamani kwa Mfalme. Ushuru huo ulisaidia kujenga
              zaidi himaya za Kifalme kwa mali na nguvu za kijeshi. Jamii za
              Kifalme zilikuwa katika hatua kubwa ya maendeleo kabla ya

              ukoloni.

              Omukama (mfalme) Rumanyika

              Omukama Rumanyika ni miongoni mwa viongozi wa kifalme
              waliotawala jamii za Buhaya. Neno Omukama lina maana ya

              Mfalme au mkubwa wa wote. Jamii ziliwatambua viongozi wake
              kwa jina hili kwa kuwa walikuwa na nguvu ya mali katika jamii.
              Wafalme walimiliki biashara, ardhi, chuma na mifugo. Jamii
              zilitegemea vitu hivi kutoka kwa Wafalme. Watu hawakuwa na

              umiliki wa ardhi na mifugo. Hivyo, walipaswa kufanya kazi kwa
              mfalme ili kupata mali na mazao. Wafalme ndio waliowapa
              watu maeneo ya kulima na pindi walipovuna, walipaswa kuleta
              sehemu ya mavuno hayo kwa Mfalme kama malipo.


              Umiliki mkubwa wa ardhi katika jamii za Kifalme ndiyo uliokuza
              mfumo wa ushirikiano na uhusiano katika jamii uliojulikana kama

              Nyarubanja. Mfumo huu ulikuwa na tabaka la Abatwazi ambao
              walimiliki ardhi, na Abatwana ambao walimilikiwa na Abatwazi



                                                   125




                                                                                          06/11/2024   11:30:21
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   125                                    06/11/2024   11:30:21
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   125
   127   128   129   130   131   132   133   134   135   136   137