Page 127 - Historiayatznamaadili
P. 127

Utawala wa himaya hii ulikua kutokana na biashara za masafa
              marefu zilizofanyika kupitia himaya yake hadi Pwani ya Bahari ya
              Hindi. Biashara hizi zilimsaidia Mtemi Isike kupata silaha imara
              na hivyo, kujenga jeshi la
          FOR ONLINE READING ONLY
              Unyanyembe, lenye nguvu,
              silaha  imara  na  mbinu  za
              kivita.  Mtemi Isike alikuwa
              na ngome imara  ya kivita

              katika ikulu ya Itetemya.
              Hii ilimwezesha kiongozi
              huyu kujilinda na kupiga
              utawala wa  Wajerumani

              walipovamia  himaya  yake
              ya Unyanyembe.  Kielelezo
              namba 2, kinaonesha picha
              ya Mtemi Isike.                         Kielelezo namba 2: Mtemi Isike



              Kiongozi huyu alipigana na Wajerumani kwa muda mrefu, zaidi
              ya miaka minne. Jeshi la Wajerumani halikuweza kumshinda.

              Aidha, Wajerumani walifanikiwa kuzingira himaya yake na
              kumvamia baada ya kusalitiwa na watu wake wa karibu. Mtemi
              Isike alijiua yeye na familia yake katika ngome yake. Mtemi Isike
              alikuwa ni kiongozi shupavu na imara, usaliti ndio ulisababisha

              kushindwa kwake.

              Mtemi (chifu) Litti Kidanka

              Mtemi Litti Kidanka ni mwanamke shujaa aliyeongoza kabila la
              Wanyaturu. Mtemi Litti alijulikana Unyaturuni kote kwa sababu ya
              nguvu na msimamo wake. Shujaa huyu hakuwa tayari kuruhusu

              wageni kuingia katika himaya yake na kuleta utamaduni wa
              kigeni. Mtemi Litti aliongoza mgomo wa Wanyaturu sehemu ya
              Kaskazini, dhidi ya Wajerumani, kutokana na ushujaa wake.

              Kiongozi huyu alipambana na Wajerumani kwa muda mrefu



                                                   120




                                                                                          06/11/2024   11:30:21
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   120                                    06/11/2024   11:30:21
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   120
   122   123   124   125   126   127   128   129   130   131   132