Page 129 - Historiayatznamaadili
P. 129

kwa jina la “Mukwavinyika” lenye maana ya “Mtemi wa ardhi”.
              Kielelezo namba 4, kinaonesha picha ya Mutwa Mkwawa.

              Kama ilivyokuwa viongozi wengine

              wa  utawala  wa  Watemi,  Mutwa
          FOR ONLINE READING ONLY
              Mkwawa alipigana vita na makabila
              mengi yaliyomzunguka ili kuongeza
              umiliki zaidi wa ardhi katika eneo
              alilotawala.


              Kiongozi huyu alikuwa na nguvu
              kubwa ya kijeshi hata kupewa jina la
              “shujaa wa vita”. Kiutawala alikuwa
              kiongozi mwenye nguvu za kivita
                                                            Kielelezo namba 4: Mutwa
              na mwenye kuheshimiwa na jamii               Mkwawa, mtemi wa Wahehe
              yake.


              Utawala wa Mutwa Mkwawa ulikua kutokana na uvamizi wa kivita
              katika maeneo yaliyowazunguka. Mfano, Mutwa Mkwawa aliweza
              kutawala eneo kubwa sana kuanzia kusini mwa Mpwapwa hadi
              Malangali karibu na Mbalali. Pia, Mutwa Mkwawa alikuwa na
              mfumo wa uongozi imara uliosaidia katika uongozi na utawala
              wake. Viongozi katika utawala huu walishirikiana ili kuongeza
              ulinzi, kutawala na kudhibiti uvamizi wa wageni. Kielelezo namba
              5, kinaonesha mfumo wa utawala wa Mutwa Mkwawa.


                       Mtemi                           Kiongozi mkuu



                       Wanamhala                    Mkutano wa wazee wa ukoo


                                                      Wakusanya kodi
                              Minula
                                                       Msimamizi masuala ya imani
                      Nganwe

                                                       Mpelelezi
                             Mtwale

                     Kielelezo namba 5: Mfumo wa uongozi wa mutwa Mkwawa


                                                   122




                                                                                          06/11/2024   11:30:21
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   122                                    06/11/2024   11:30:21
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   122
   124   125   126   127   128   129   130   131   132   133   134