Page 133 - Historiayatznamaadili
P. 133

na kulazimika kuleta sehemu ya mazao kwa Abatwazi kama
              malipo. Shughuli za kilimo ziliimarisha tawala za Kifalme.


              Jamii za Buhaya chini ya Omukama Rumanyika, pia, zilikuwa na
              umaarufu katika kufua chuma. Hii ilisaidia kukua kwa utawala
          FOR ONLINE READING ONLY
              huu kutokana na jamii zingine kuhitaji zana za chuma kwa wingi.
              Jamii za Buhaya na Karagwe zilibadilisha zana za chuma ili
              kupata bidhaa zingine. Jamii hizi zilifanya biashara  na jamii

              kama vile Wanyamwezi, Wasukuma na Waha. Pia, zilifanya
              biashara na jamii za mbali, Mfano, falme za Uganda kama vile,
              Bunyoro na Ankole na maeneo ya Buganda ili kupata ng’ombe.


              Aidha, ukuaji wa tawala za kifalme ulisababishwa na uwapo
              wa mfumo imara wa uongozi. Kielelezo namba 6, kinaonesha

              mfumo wa uongozi wa Kifalme.


                       Omukama                       Kiongozi mkuu (mfalme)


                         Katikiro                   Waziri mkuu

                                                         Mawaziri
                            Batongole
                                                           Baraza la washauri
                               Lukiko
                                                            Wakuu wa eneo (mkoa)
                            Bami B’enshonzi
                                                                 Mwenyekiti wa kijiji
                                    Bakungu

                Kielelezo namba 6: Mfumo wa uongozi, tawala za kifalme (Buhaya)


              Mfano wa mfumo huu wa utawala ulikuwapo katika jamii za
              Wapare, ambapo  kiongozi  mkuu  alikuwa  Mfumwa (chifu)
              akifuatiwa na baraza la wazee Mnjama, Wakuu wa vijiji Chila
              au Mchili na chini walikuwapo walinzi na askari.








                                                   126




                                                                                          06/11/2024   11:30:21
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   126                                    06/11/2024   11:30:21
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   126
   128   129   130   131   132   133   134   135   136   137   138