Page 137 - Historiayatznamaadili
P. 137

FOR ONLINE READING ONLY




















                   Kielelezo namba 8: Mangi wakiwa katika boma la Wajerumani


                      Zoezi namba 1

                1.  Eleza mambo uliyojifunza kutokana na mfumo wa

                      uongozi wa Kifalme, Kitemi na Mangi.
                2.  Taja sababu zilizosababisha Wafalme, Mangi na Watemi
                      kuwa na nguvu kubwa katika jamii walizozitawala.




              Umwinyi Pwani ya Afrika Mashariki

              Utawala wa Umwinyi ulishamiri sehemu za Pwani hasa katika
              maeneo ya Kilwa, Mafia na Bagamoyo. Pia, ulikuwepo maeneo

              ya Unguja na Pemba kwa upande wa Zanzibar. Watawala
              hawa walijulikana kwa majina tofauti kufuatana na sehemu
              walizozitawala. Watawala walioishi sehemu za kati, Magharibi
              na Kusini ya Unguja walijulikana kama Mwinyi Mkuu ikiwa na
              maana ya mkuu wa eneo. Watumbatu waliwaita Sheha na

              Pemba waliitwa Madiwani au Wajumbe.






                                                   130




                                                                                          06/11/2024   11:30:22
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   130
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   130                                    06/11/2024   11:30:22
   132   133   134   135   136   137   138   139   140   141   142