Page 141 - Historiayatznamaadili
P. 141

kiuchumi na kijamii. Pia, zilikuwa na mamlaka katika maeneo
              yao na watu waliowatawala.

              Viongozi walisaidia katika kukusanya ushuru kutoka kwa
              wafanyabiashara waliopita na kufanya biashara katika maeneo
          FOR ONLINE READING ONLY
              yao na kuutumia kuimarisha himaya zao. Aidha, mamlaka za
              jadi zilifanya biashara zenye faida kwa watu wao. Hii ilisaidia
              jamii hizi kuwa na nguvu za uchumi. Pia, mamlaka za jadi
              zilihamasisha shughuli za uzalishaji mali. Hii ilisaidia jamii zao
              kuzalisha bidhaa kwa ajili ya matumizi na kuwa na ziada ambazo
              ziliwezesha biashara. Ziada ilitumika katika biashara ili kupata
              bidhaa zilizokosekana kwao. Hii ilisababisha maendeleo ya jamii
              zao.

              Vilevile, mamlaka za jadi zilikuwa na mchango mkubwa sana
              katika kukuza maadili ya jamii zao. Viongozi hawa walisimamia
              maadili katika jamii yao kama vile, heshima, kufanya kazi kwa bidii,
              ushirikiano, upendo, usawa na umoja.  Pia, walikuwa wasuluhishi
              wa migogoro ndani ya jamii zao. Watu wote waliokwenda kinyume
              na maadili ya jamii walichukuliwa hatua kwa kupewa adhabu.

              Aidha, mamlaka za jadi zilisimamia ustawi wa watu na jamii.
              Mfano, matumizi bora ya rasilimali, kama vile maji, ardhi na
              misitu. Pia, walikuwa ni viongozi wa dini. Hivyo, walisimamia
              miungu ya jamii zao. Mamlaka za jadi zilisimamia na kuhakikisha
              ulinzi na usalama wa jamii zao na masuala ya mila na utamaduni
              katika eneo lao.

              Kimsingi, mfumo wa utawala wa mamlaka za kijadi ulikuwa na
              mchango mkubwa sana katika maendeleo ya kijamii. Mamlaka
              za jadi zilikuwa na utamaduni mzuri wa kutawala kwa kugawana
              madaraka. Mgawanyo wa madaraka ulileta mafanikio katika
              ulinzi na kuwapatia wanajamii mahitaji yao ya msingi. Pia,
              mifumo hii ya utawala ilitumika kutatua migogoro katika jamii

              na kusimamia ulinzi na usalama wa jamii.

                                Kazi ya kufanya namba 12

                           Andika mambo uliyojifunza kuhusu mamlaka za jadi na
                           jinsi ya kuyaendeleza ili kuboresha uongozi wa sasa.




                                                   134




                                                                                          06/11/2024   11:30:22
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   134                                    06/11/2024   11:30:22
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   134
   136   137   138   139   140   141   142   143   144   145   146