Page 139 - Historiayatznamaadili
P. 139

rika mbili muhimu: wazee na vijana. Wazee ndio waliokuwa na
              madaraka ya mwisho kabisa katika jamii ya Wamasai. Kiongozi
              wa kundi la wazee alijulikana kama Olaiboni, kundi hili lilitoa
              ushauri  kwa  makundi  mengine  na  hakuna  kitu  kilichokuwa
          FOR ONLINE READING ONLY
              kinaweza kufanyika katika jamii bila idhini ya rika hili la wazee.
              Pia,  kundi  hili  la  wazee  lilikuwa  na  wajibu  wa  kusuluhisha
              migogoro iliyokuwa inatokea katika jamii yao. Kundi la vijana
              lilijulikana kama morani na lilihusisha vijana wenye umri kati ya

              miaka 18 na 35. Kundi hili ndilo lililokuwa nguvukazi ya jamii.
              Kundi hili lilihusika na ufugaji kama vile, kutafuta maji na malisho
              ya mifugo yao. Pia, walikuwa ndio walinzi wa mali na usalama
              wa jamii nzima. Morani walitegemea sana ushauri wa wazee

              chini ya Olaiboni katika kutekeleza majukumu yao. Aidha, wazee
              chini ya Olaiboni ndio waliokuza na kutunza maadili ya jamii hizi.


              Utawala wa kiukoo

              Baadhi ya jamii kabla ya ukoloni zilikuwa zinajitawala katika
              ngazi ya ukoo. Jamii hizi ni zile ambazo hazikuwa zimefika hatua
              ya kuunganisha koo mbalimbali na kupata himaya za Uchifu na
              Ufalme. Jamii hizi ziliongozwa na mkuu wa ukoo. Wakuu wa

              ukoo walijulikana kwa majina tofauti tofauti kulingana na koo zao.
              Jamii zilizokuwa na utawala wa kiukoo ni zile zilizoishi maeneo
              ya Kusini Mashariki mwa Tanzania. Mfano wa jamii hizo ni:
              Wamatumbi, Wamwera, Wangido, Wamakonde, Wandendeule,

              Wakisi, Wapangwa na Wamakua.

              Kimsingi, jamii za kabla ya ukoloni zilikuwa na mamlaka za

              uongozi imara zilizotawala jamii kisiasa, kiuchumi na kimaadili.
              Mamlaka hizi zilikuwa na nguvu imara za uongozi na ulinzi.
              Hivyo, kuweza kuongoza na kulinda himaya zao.  Mamlaka za
              jadi zilitofautiana kati ya kabila na kabila. Kielelezo namba 9,
              kinaonesha mtawanyiko wa baadhi ya makabila nchini.







                                                   132




                                                                                          06/11/2024   11:30:22
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   132
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   132                                    06/11/2024   11:30:22
   134   135   136   137   138   139   140   141   142   143   144