Page 135 - Historiayatznamaadili
P. 135

Sababu za ukuaji wa tawala za Mangi
              Uwepo wa ardhi yenye rutuba na mvua za kutosha ilikuwa sababu
              mojawapo ya kukua kwa tawala za Mangi kabla ya kuja kwa
              ukoloni. Jamii hizi zipo karibu na Mlima Kilimanjaro, maeneo
          FOR ONLINE READING ONLY
              yenye mvua za kutosha na udongo wenye rutuba. Jamii hizi
              zilijishughulisha na kilimo. Hivyo, ardhi ilikuwa kichocheo kikubwa
              cha maendeleo na uchumi. Pia, ugunduzi wa chuma ulisaidia
              kukua kwa tawala za Mangi. Jamii hizi zilitumia zana za chuma

              katika kilimo kama vile majembe, mapanga, mundu na mashoka
              kutoka jamii za Ugweno. Matumizi ya zana za chuma katika kilimo
              yalisaidia maendeleo ya kilimo. Jamii za Wachaga zililima na
              kupata mazao ya chakula na ziada. Ziada zilitumika kwa ajili
              ya biashara. Jamii hizi zilifanya biashara na jamii za Wapare,
              Wakamba na Wasambaa kwa kubadilishana mazao ya chakula

              ili kupata zana za chuma na bidhaa zingine.

              Jamii za Kimangi, kama zilivyokuwa jamii za Kitemi, zilijenga
              himaya zao kutokana na kupigana na koo zingine ili kuongeza

              himaya. Hii ilisababisha vita kati ya jamii hizi mara kwa mara.
              Mfano, Mangi Sina wa Kibosho alipigana na Mangi Marealle
              wa Marangu mara kwa mara. Mangi Sina alipigana na Mangi
              wa Machame. Vita hivyo vilikuwa na lengo la kuongeza himaya
              zao. Kiongozi aliyeshindwa alinyang’anywa ardhi na mifugo na

              himaya yake ilichukuliwa na Mangi mwingine. Watawala wenye
              nguvu ndio walioshika maeneo makubwa ya utawala. Ujio wa
              wakoloni ulikuta tawala za Mangi zikiwa na maendeleo katika
              kilimo, biashara na ufugaji. Pia, zilikuwa na nguvu kubwa ya
              kijeshi. Mfano, Mangi Meli alikuwa na jeshi imara katika himaya
              yake ya Old Moshi. Hivyo, kupinga utawala wa Wajerumani

              katika eneo lake.

              Mangi Meli

              Mangi Meli alipinga uvamizi wa Wajerumani katika himaya yake
              kutokana na uimara wa jeshi lake. Kielelezo namba 7, kina picha

              ya Mangi Meli.

                                                   128




                                                                                          06/11/2024   11:30:21
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   128                                    06/11/2024   11:30:21
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   128
   130   131   132   133   134   135   136   137   138   139   140