Page 134 - Historiayatznamaadili
P. 134

Kazi ya kufanya namba 8

                           Chunguza mchoro wa mfumo wa uongozi wa jadi

                           wa jamii za Kifalme na Kitemi, kisha eleza mfanano
                           na tofauti zilizopo katika mgawanyo wa madaraka
          FOR ONLINE READING ONLY
                           katika mifumo hiyo.


              Mgawanyo wa madaraka ulileta mafanikio mengi katika jamii
              za kale. Mgawanyo huu ulisaidia kushirikisha watu mbalimbali
              katika uongozi. Hivyo, kuwezesha shughuli za jamii na watu

              kupata mahitaji yao ya msingi. Pia, mfumo wa uongozi ulitumika
              kutatua migogoro katika jamii na kusimamia ulinzi na usalama
              wa jamii.


              Licha ya Mfalme, Rumanyika, mkoa wa Kagera ulikuwa na
              watawala wengine kama Kasusura aliyetawala Biharamulo,

              Rutinwa aliyetawala Kiziba na Kayoza aliyetawala Bugabo. Pia,
              palikuwa na watawala wengine kama Kahigi aliyetawala Kihanja,
              Nyarubamba aliyetawala Ihangiro, Lugomola aliyetawala Bukara,
              na Rukamba aliyetawala Kyamtwara. Hawa walikuwa na utawala
              wa kifalme katika maeneo yao.


                                Kazi ya kufanya namba 9

                           Andika sababu za kukua na kuimarika kwa utawala
                           wa kifalme kabla ya kuja kwa ukoloni nchini.





              Utawala wa Mangi katika jamii za Wachaga
              Utawala wa Mangi ni miongoni mwa tawala za Kichifu zilizokuwapo
              katika mkoa wa Kilimanjaro, Kaskazini mwa Tanzania katika jamii

              za Wachaga. Mfano, Mangi Sina alitawala eneo la Kibosho, Mangi
              Marealle eneo la Marangu na Vunjo, Mangi Shangali eneo la
              Machame na Mangi Meli eneo la Old Moshi. Uongozi wa Mangi
              ulikuwa wa kurithi.




                                                   127




                                                                                          06/11/2024   11:30:21
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   127
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   127                                    06/11/2024   11:30:21
   129   130   131   132   133   134   135   136   137   138   139