Page 136 - Historiayatznamaadili
P. 136

Mangi Meli aliua baadhi ya Wajerumani na kamanda wao
              aliyeitwa       Von      Bulow.
              Wajerumani walishindwa vita
              na waliondoka katika himaya
          FOR ONLINE READING ONLY
              yake eneo la Old Moshi kwa
              muda wa mwaka mmoja na
              nusu. Aidha,  Wajerumani
              walirudi kupigana  naye

              baada ya kujiimarisha kijeshi.
              Hata hivyo, ilibidi Wajerumani
              kutumia jeshi la Wanubi
              kutoka Sudani katika jeshi

              lao ili kukabiliana na Mangi  Kielelezo namba 7: Mangi Meli
              Meli.                                           wa Old Moshi


              Wanubi ni Waafrika na ni watu wa vita. Vita hivi vilidumu siku

              mbili tu na Wajerumani walifanikiwa kuingia eneo lake. Mangi
              Meli alikubali kwa shingo upande Wajerumani kuingia katika
              himaya yake. Aidha, Mangi Meli aliendelea kwa siri kujijenga
              kijeshi ili kuwaondoa Wajerumani katika eneo lake. Kiongozi
              huyu alihamasisha jamii za Wachaga, Wameru, Wamasai, na

              Wapare kuungana kijeshi ili kupinga Wajerumani kuingia katika
              maeneo yao. Aidha, mpango huu haukufanikiwa kwa sababu
              alisalitiwa na wenzake. Wajerumani walimkamata na kumhukumu

              kifo cha kunyongwa hadharani. Hivyo, Mangi Meli alinyongwa
              hadharani. Mangi Meli alikuwa kiongozi imara na shupavu, kama
              siyo usaliti kutokana na ulaghai wa Wajerumani, kamwe Mangi
              Meli asingeshindwa vita na kukamatwa.


              Kuna Mangi wengine ambao walipinga utawala wa Wajerumani
              kwa nyakati tofauti. Kielelezo namba 8, kinaonesha picha ya
              baadhi ya Mangi wakiwa katika eneo la boma la Wajerumani

              kujibu shitaka la kupinga utawala wa Wajerumani.




                                                   129




                                                                                          06/11/2024   11:30:21
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   129                                    06/11/2024   11:30:21
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   129
   131   132   133   134   135   136   137   138   139   140   141