Page 131 - Historiayatznamaadili
P. 131

Tawala za Kifalme kabla ya ukoloni
              Tawala za Kifalme zilikuwa maarufu katika maeneo ya Kaskazini
              Magharibi mwa Tanzania, pembeni mwa Ziwa Victoria. Utawala

              wa Kifalme ulijikita katika jamii za maeneo ya Karagwe na Buhaya.
          FOR ONLINE READING ONLY
              Utawala wa Kifalme ulikuwa wa kurithi na ulianzia katika utawala
              wa Bachwezi na Babiito. Utawala ambao uliibuka zaidi wakati wa

              biashara ya masafa marefu na wafanyabiashara toka Mashariki
              ya Mbali na Kati hasa Waarabu. Utawala wa Kifalme uliisha
              baada ya kufutwa kwa tawala za Kifalme na Kichifu nchini na
              Rais wa kwanza wa Tanzania, Hayati Mwalimu Julius Kambarage
              Nyerere.


              Mambo yaliyosababisha kukua kwa tawala za Kifalme nchini

              Utawala wa Kifalme ulikua kutokana na shughuli za kilimo. Hii
              ilitokana na uwepo wa ardhi nzuri yenye rutuba na mvua za
              kutosha katika eneo la utawala wa Kifalme. Jamii za Kifalme

              zilijishughulisha sana na shughuli za kilimo cha mazao ya chakula,
              na hata kuzalisha ziada ambayo ilitumika kwa ajili ya biashara na
              jamii zilizowazunguka.


              Ugunduzi wa chuma wakati wa utawala wa “Ndagara” katika
              maeneo ya Karagwe kulichangia zaidi kukua kwa himaya za
              Kifalme maeneo ya Buhaya na Karagwe kabla ya ukoloni.
              Ugunduzi huo ulisababisha kukua kwa viwanda vya ufuaji chuma

              na kutengeneza zana imara za kilimo kama vile majembe,
              mashoka, mapanga na mundu. Zana hizi zilichangia kuongeza
              maendeleo katika shughuli za kilimo, kwani wakulima waliweza

              kulima maeneo makubwa zaidi na kupata mazao ya chakula na
              ziada kwa ajili ya biashara.

              Vilevile, ugunduzi wa chuma ulisaidia jamii hizi kutengeneza

              zana za vita na uwindaji kama vile mishale, mikuki na mapanga.
              Zana hizi zilitumika kwa ajili ya ulinzi na upanuzi wa himaya za
              Kifalme. Pia, zilitumika katika biashara ili kupata bidhaa ambazo



                                                   124




                                                                                          06/11/2024   11:30:21
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   124                                    06/11/2024   11:30:21
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   124
   126   127   128   129   130   131   132   133   134   135   136