Page 128 - Historiayatznamaadili
P. 128

bila kushindwa kutokana na
              mbinu za kivita alizokuwa
              nazo. Alitumia nyuki na silaha
              za jadi kushinda vita dhidi ya
          FOR ONLINE READING ONLY
              wavamizi katika eneo lake.
              Mtemi huyu alitumia nguvu
              za asili kuwakusanya nyuki
              na kuwatuma kuyazingira

              majeshi ya Wajerumani
              waliomwendea kwa lengo la
              kumuua.  Kielelezo namba
              3, kinaonesha Mtemi Litti                Kielelezo namba 3: Mtemi Litti

              Kidanka.                                             Kidanka

              Nyuki walitumwa kila majeshi ya Wajerumani yalipomkaribia
              na kuikaribia  himaya  yake.  Nyuki  hao  waliwauma  majeshi
              hayo kulingana na maagizo ya mtemi huyu. Hivyo, Wajerumani
              walikimbia ili kuokoa maisha yao. Mapambano dhidi ya
              Wajerumani  yalichukua  zaidi  ya  miaka  mitatu.  Mtemi  Litti
              alipambana na Wajerumani mara mbili na kuwashinda. Safari
              ya tatu Mtemi Litti hakuweza kufanikiwa kuwashinda kutokana

              na usaliti uliofanywa na baadhi ya maadui zake. Hii ilisababisha
              Wajerumani kufanikiwa kumuua na kukata kichwa chake na
              kukipeleka Ujerumani na hakijarejeshwa nchini hadi leo.

                                Kazi ya kufanya namba 5


                           Jadili madhara ya usaliti katika ulinzi na usalama wa
                           jamii zetu hapo kale na sasa.




              Mutwa (mtemi) Mkwawa
              Mutwa Mkwawa Mukwavinyika Mwamuyinga alikuwa mtawala
              wa jamii ya Wahehe. Milki ya utawala wa Mutwa Mkwawa ilikuwa

              katika Mkoa wa Iringa, eneo la Kalenga. Kiongozi huyu alijulikana




                                                   121




                                                                                          06/11/2024   11:30:21
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   121
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   121                                    06/11/2024   11:30:21
   123   124   125   126   127   128   129   130   131   132   133