Page 123 - Historiayatznamaadili
P. 123

Kwa  mfano  walijulikana  kwa  majina  ya  Abakama,  Watwa,
              Mangi, Watemi na kadhalika. Viongozi hawa waliheshimika sana
              katika himaya zao. Hii ni kwa sababu ya umaarufu na nguvu
              zilizotokana na uhodari wa vita, umiliki wa maeneo makubwa na
              yenye rasilimali za jamii, nguvu za asili na utawala. Hapakuwapo
          FOR ONLINE READING ONLY
              na mtu aliyeweza kuwapinga watawala hawa kutokana na nguvu
              na mamlaka walizokuwa nazo.


              Viongozi hawa walipatikana kupitia uchaguzi, urithi, ushupavu
              wa kivita na umaarufu wa mtu katika kutenda kazi au uganga.
              Aidha, kiongozi katika jamii alipaswa awe ni mpenda watu, awe
              na tabia njema na anapenda kufanya kazi kwa bidii. Pia, ilikuwa
              mwiko kwa jamii kutawaliwa na mtu mvivu, asiyependa watu au

              mwenye tabia mbaya.

                                Kazi ya kufanya namba 2


                           Jadili mambo yanayofanana na kutofautiana katika
                           uchaguzi wa viongozi wa sasa na wa kabla ya
                           ukoloni.



              Utawala wa viongozi wa jadi katika jamii

                                Kazi ya kufanya namba 3


                           Soma matini mbalimbali ikiwemo maktaba mtandao
                           kuhusu mamlaka za jadi katika jamii za Kitanzania
                           kabla ya ukoloni.



              Utawala wa Watemi

              Mfumo wa Kitemi ulianza katika jamii za Wanyamwezi. Baadaye
              ulisambaa katika maeneo ya Usukuma, Usangu, Uhehe, Ukimbu,
              Ugogo, Ubena na maeneo mengine ya nchi. Uongozi huu ulitumia
              jina “Mtemi” kutokana na namna mamlaka zilivyoundwa. Neno
              mtemi linatokana na neno “kutema” lenye maana ya “kukata” kwa
              ajili ya kuongeza ardhi mpya. Jamii zilizokuwa na mamlaka za



                                                   116




                                                                                          06/11/2024   11:30:20
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   116
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   116                                    06/11/2024   11:30:20
   118   119   120   121   122   123   124   125   126   127   128