Page 125 - Historiayatznamaadili
P. 125

Baadhi ya viongozi wa jadi waliokuwa na mfumo wa Watemi ni
              Mtemi Mirambo wa Unyamwezi, Isike wa Unyanyembe, Mkwawa
              wa Uhehe na Mazengo wa Ugogo. Hawa ni baadhi tu ya viongozi
              wa jadi waliotumia mfumo wa utawala wa Watemi.
          FOR ONLINE READING ONLY
              Mtemi Mirambo

              Mtemi Mirambo alikuwa kiongozi wa jamii ya Wanyamwezi (1840
              – 1880). Utawala wa Mtemi Mirambo ulikuwa wa kurithi kutoka kwa
              baba yake Mtemi Kasanda wa Uyowa. Uyowa ni eneo la utawala
              wa baba yake. Kielelezo namba 1 kinaonesha picha ya Mtemi
              Mirambo.


              Tangu awali himaya hii ilikua kutokana na uwezo mkubwa wa
              kijeshi waliokuwa nao. Aidha, utawala huu ulikua zaidi kutokana
              na uvamizi wa maeneo yaliyowazunguka ili kupanua himaya.
                                                          Mfano, Mtemi Mirambo
                                                          aliendeleza utawala wa

                                                          himaya hii baada ya kifo
                                                          cha baba yake kwa kuvamia
                                                          maeneo yaliyowazunguka
                                                          kama vile Ulyankulu na
                                                          kuunganisha na Uyowa,
                                                          hivyo kuanzisha utawala wa
                                                          Urambo.


                                                          Kama zilivyo tawala zingine
                                                          za Kitemi, utawala huu
                                                          uliimarika zaidi kutokana
                                                          na biashara za masafa
                                                          marefu na zile zilizofanyika
                                                          katika  Pwani ya  Bahari
                                                          ya Hindi. Jamii hii ya

                                                          Wanyamwezi ilikuwa moja
                                                          ya jamii maarufu sana
                                                          katika biashara.
                Kielelezo namba 1: Mtemi
                            Mirambo

                                                   118




                                                                                          06/11/2024   11:30:20
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   118
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   118                                    06/11/2024   11:30:20
   120   121   122   123   124   125   126   127   128   129   130