Page 121 - Historiayatznamaadili
P. 121

Zoezi la jumla

               1.  Je, ni kwa nini mfumo wa ujima uliweza kujenga misingi
                     ya haki na usawa katika jamii?
               2.  Ni mambo yapi yalisababisha kuvunjika kwa misingi ya
                     haki na usawa wakati wa mfumo wa ukabaila katika jamii
          FOR ONLINE READING ONLY
                     kabla ya ukoloni?

               3.  Fafanua sababu za kuzuka uhusiano wa kibiashara baina
                     ya jamii za Watanzania kabla ya ukoloni.
               4.  Taja mabadiliko ya kiuchumi yaliyosababishwa na kukua
                     kwa biashara ya masafa marefu kabla ya ukoloni.
               5.  Ni mabadiliko yapi ya kijamii yaliyosababishwa na kukua
                     kwa biashara ya masafa marefu kabla ya ukoloni?

               6.  Je, ni kwa namna gani biashara za masafa marefu
                     zilisababisha kukua kwa shughuli za kiuchumi kabla ya
                     ukoloni?
               7.  Bainisha sababu ya kuimarika kwa tawala za kijamii wakati
                     wa biashara ya masafa marefu na wageni toka Mashariki

                     ya Kati.


              Msamiati

              Biashara ya                 biashara iliyokuwa ikifanywa na jamii za
              masafa marefu               kale baina ya Pwani na maeneo ya ndani
                                          ya Tanzania

              Dola                        mamlaka katika eneo fulani, mathalani
                                          katika nchi

              Karne                       muda wa miaka mia moja

              Mwinyi                      kiongozi au mtu aliyekuwa na heshima na
                                          dhamana ya uongozi na utawala katika
                                          maeneo ya ukanda wa Pwani

              Mtwana                      mtu aliyekuwa chini ya Mwinyi na
                                          aliwajibika kumtumikia

              Ushuru                      ni kodi inayotozwa kwa bidhaa au shughuli
                                          maalumu



                                                   114




                                                                                          06/11/2024   11:30:19
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   114
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   114                                    06/11/2024   11:30:19
   116   117   118   119   120   121   122   123   124   125   126