Page 116 - Historiayatznamaadili
P. 116

Wafipa. Wafipa na Wakinga walikuwa maarufu kwa uhunzi.
              Hivyo, walibadilishana bidhaa za chuma na Wakisi ili kupata
              bidhaa za ufinyanzi na samaki kutoka ziwa Nyasa. Ubora wa

              vyungu vya Wakisi uliwawezesha kufanya biashara mpaka
          FOR ONLINE READING ONLY
              Malawi. Wanyakyusa  walibadilishana  mazao  ya  chakula  ili

              kupata bidhaa zingine.

              Sehemu za Magharibi na Kaskazini Magharibi mwa Tanzania,

              jamii  za Wanyamwezi, Wahaya na  Wasukuma zilikuwa  maarufu
              katika biashara hii. Ushirikiano na uhusiano wa kibiashara
              ulikuwapo  baina  ya  jamii  za  Wasukuma,  Wanyamwezi  na

              Wahaya. Biashara hii baadaye ilikwenda hadi maeneo ya nchi
              za Burundi, Rwanda, Bunyoro, Buganda na Kongo (Katanga) ya

              leo. Bidhaa katika biashara hii zilikuwa chumvi kutoka Uvinza,
              zana za chuma kutoka Karagwe na Bunyoro, shaba kutoka
              Katanga, kahawa kutoka Buhaya na nguo za miwale kutoka

              Kongo. Chumvi ya Uvinza ilikuwa maarufu sana kama bidhaa
              katika biashara hii. Biashara za masafa marefu zilisababisha
              kukua kwa shughuli za uchumi zilizochochewa na uhitaji wa

              bidhaa katika biashara. Kielelezo namba 3, kinaonesha njia za
              biashara za masafa marefu.


              Biashara za Masafa Marefu Pwani ya Bahari ya Hindi

              Ushirikiano na uhusiano wa biashara za masafa marefu ulikuwa

              zaidi hadi kuhusisha jamii za Pwani ya Bahari ya Hindi. Ujio
              wa wageni kutoka Mashariki ya Mbali na Kati katika maeneo
              ya Pwani ya Bahari ya Hindi ulisababisha wafanyabiashara

              wakubwa, hasa waliomiliki biashara za masafa marefu kuanza
              kufanya biashara na wageni hao. Hii ilisababisha kukua zaidi

              kwa ushirikiano na uhusiano wa kibiashara nchini.







                                                   109




                                                                                          06/11/2024   11:30:18
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   109
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   109                                    06/11/2024   11:30:18
   111   112   113   114   115   116   117   118   119   120   121