Page 114 - Historiayatznamaadili
P. 114

Jamii za wachongaji zilibadilishana bidhaa kutoka kwa wahunzi
              na wakulima kutoka kwa wafugaji. Wahunzi vivyo hivyo,
              walibadilishana bidhaa zao kwa nafaka kutoka kwa wakulima,
              wachongaji na wafugaji. Wakulima walibadilishana mazao na
          FOR ONLINE READING ONLY
              wahunzi ili kupata zana za kilimo. Pia, wakulima walibadilisha
              mazao yao na jamii za wawindaji ili kupata mawindo kutoka kwa
              wawindaji. Pia, wawindaji walibadilishana mawindo na wahunzi
              ili kupata zana za chuma kama vile mikuki, mishale na visu.

              Uhitaji katika jamii ndio uliosababisha ushirikiano na uhusiano
              katika jamii kwa lengo la kupata bidhaa zilizokosekana katika
              jamii zao. Biashara hizi awali zilifanyika kwa lengo la kujikimu
              na siyo kupata faida kama ilivyo sasa.


              Aidha, kadiri muda ulivyozidi kwenda, baadhi ya vitu vilianza
              kutumika kama kipimo katika ubadilishanaji. Mfano wa bidhaa
              zilizochukua hadhi ya vipimo ni zana za chuma na chumvi.

              Bidhaa hizi zilitumika kama vile itumikavyo fedha sasa. Hii ni
              kwa  sababu  kila  mtu alihitaji bidhaa hizi. Mfano, idadi fulani
              ya zana za chuma (majembe, mashoka, mapanga, mikuki)

              ilitumika kununulia mifugo na nafaka mbalimbali. Hivyo, watu
              walilinganisha thamani ya bidhaa na kubadilishana.  Jamii
              ziliweza kujitosheleza katika mahitaji ya chakula na uzalishaji
              mali kama ilivyo sasa. Kimsingi, ushirikiano na uhusiano huu kwa
              kiasi kikubwa ulikuza shughuli za biashara kabla ya ukoloni. Hali

              hii ilipanua wigo kutoka biashara kati ya jamii za jirani mpaka
              jamii za mbali. Jamii zilianza kusafiri hadi jamii zingine kufanya
              biashara, hivyo kukua kwa biashara za masafa marefu katika

              jamii.


              Biashara za masafa marefu
              Ushirikiano na uhusiano huu ulitambulika kama biashara za

              masafa marefu kwa sababu, jamii moja ilisafiri umbali mrefu ili
              kubadilishana bidhaa zilizokosekana katika jamii zao. Biashara




                                                   107




                                                                                          06/11/2024   11:30:18
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   107                                    06/11/2024   11:30:18
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   107
   109   110   111   112   113   114   115   116   117   118   119